Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

KUKATIKA KWA DARAJA KATAVI

NA,GOODLUCK CHRISTOPHER
Kufuatia mvua kubwa inayo endelea kunyesha mkoani Katavi imepelekea kukatika kwa daraja la mto Makongoro linalo unganisha mitaa ya kijiji cha Isubangala kata ya ilangu katika wilaya ya Tanganyika daraja ambalo ni tegemezi kwa wananchi wa kijiji hicho na maeneo jirani.

Aidha nimebahatika kuzungumza na mkazi wa kijiji hicho  Living Atanaz ambae amesema kuwa kukatika kwa daraja hilo ni adha kubwa kwa wakazi kwani wanashindwa kuvuka upande wapili ili kupata huduma za msingi katika maeneo kama Zahanati,Sokoni,Shuleni pamoja na Mashambani.

Kamera iliwanasa wanafunzi pamoja na watu wazima wakiwa wameshindwa kuvuka richa ya wananchi hao kujaribu kutengeneza  kivuko cha muda kwa kutumia miti jambo ambalo bado lina leta hofu kwa wakazi hao.

Hata hivyo wananchi wameiomba serikali kuingilia kati suala hili haraka iwezekanavyo ili kunusuru maisha ya wakazi wa kijiji hicho pamoja na vijiji jilani ili shughuli ziweze kuendelea kama awali.

Nimegonga hodi katika ofisi za viongozi kijijini hapo ili kuzungumza nao juu ya suala hili bila mafanikio kwani tayari muda ulikua umekwisha na ofisi hizo zilikua zimekwisha kufungwa.






Chapisha Maoni

0 Maoni