Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

KIGOMA YA LEO

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Nimatumaini yangu umzima waafya na kama kawaida tunakutana tena katika makala nyingine tena lengo ikiwa ni kupeana elimu kwa kile usicho kijua na kama unakijua basi tunakuongezea maarifa napenda kukukaribisha wewe pamoja na jirani yako kwani mambo mazuri yanapatikana huku karibu sana.

Kigoma ni moja kati ya mikoa zaidi ya 30 katika nchi ya Tanzania, Mkoa huu unapatikana magharibi mwa nchi ya Tanzania huku ukiwa umezungukwa na mikoa ya Tabora,Katavi,Kahama pamoja na Kagera.

Mkoa huu una patikana pia mpakani mwa nchi kama Rwanda,Burundi pamoja na Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo hivyo huwa ni rahisi kwa watanzania kusafiri kwenda nchi hizo ama watu kutoka nchi hizo kuingia Tanzania.

Kwa asili mkoa huu una makabira  ambayo ni Waha,Wamanyema,Watongwe, wabwali, Wajiji n.k huku yakifatiwa na makabira machache mengine kutoka mikoa mingine ya Tanzania Lakini pia wakimbizi kutoka nchi ya Kongo,Burundi pamoja na Rwanda.

Mkoa wa Kigoma una wilaya zisizo pungua………… ambazo ni Halimashauri ya manispaa ya kigoma ujiji, Kasulu, Buhigwe, Kibondo pamoja na Uvinza na zote hizi zikiwa zina ukamilisha mkoa wa kigoma.

Mkoa huu umejaliwa vivutio vingi vya utali ambavyo ni Milima unayo uzunguka mji wa kigoma,Ziwa,Mbuga za wanyama, Chuvi, Mto maragalasi,Vyura wanao nyonyesha nah ii ikiwa ni maajabu makubwa sana na vingine vingi vinavyo patikana.

Shughuli zinazo fanywa na wakazi wa mkoa huu ni Kilimo,Uvuvi,Ufugaji na kazi za viwandani pamoja na maofini lengo ikiwa ni kujipatia kipato kama ilivyo kwa mikoa mingine.

Ziwa Tanganyika ni ziwa pekee linalo patikana mkoani kigoma na likiwa ni ziuwa pekee lenye kina kirefu duniani, Mbali na ziwa hili kupatikana sehemu kubwa ya kigoma limepakana pia na mikoa kama Ktavi na sehemu ndogo sana ya mkoa wa Mbeya huku ukipakana na nchi jirani kama Kongo,Burundi na Zambia.

Ziwa Tanganyika linasifiwa kwa kuzalisha samaki wengi na wazuri kama migebuka,Dagaa wa kigoma n.k ambao wanatoa furusa ya ajira kwa vijana wengi wa mkoa huu pamoja na kupata kitoweo kizuri kwa wakazi wa mkoa huu na nchi kwa ujumla.

Mv.Lyemba ni moja kati ya meli kongo ambayo imekuwa ikifanya safari zake ndani ya ziwa Tanganyika kwa kuwasafirisha watu pamoja na mizigo kati ya mkoa wa kigoma kwenda nchi jirani kama Burundi, Kongo na Zambia toka enzi za mkoroni.

Kama ilivyo kilimo ni uti wa mgongo basi wakazi wa mkoa huu kilimo ni sehemu ya maisha yao ambapo watu hujishughulisha na kilimo kwa asilimia kubwa hususa ni maeneo ya vijijini kwasababu mkoa huu una aridhi ya kusiwisha mazao mbalimbali kama Mahindi,Maharage,Kahawa,Tangawizi,Michikichi na mazao mengine mengi.

Vivutio vya utali basi kigoma ndo mahali pake kama nilivyo kutajia pale juu na kubwa zaidi ikiwa nimbuga za wanyama kama Gombe mbuga inayopatikana juub ya milima inayo lizunguka ziwa Tanganyika na ikiwa imesheheni wanyama aina ya Sokwe mtu.

Lakini pia Mahale nayo pia ni hifadhi ya wanyama pori ambayo pia imelizinguka ziwa Tanganyika ambapo watalii wengi hupenda kufika huko kwa kutumia usafiri wa Boti huku wakijionea manzali nzuri ya ziwa lenye kina kirefu duniani pamoja na samaki wa aina tofauti tofauti.

Hivyo ni baadhi ya vivutio vinavyo patikana mkoa huu wa kigoma ambavyo watalii kutoka nje na ndani huja kujionea huku seerikali ikiingiza mapato kwaajili ya utali wandani na nje.

Mji wa Ujiji ni moja ya mji mkongwe ambapo ni sehemu ya kihistoria ambapo Dkt.Living Stone alipata kuishi katika eneo hili lakini pia sehemu aliyo pata kuishi mpaka leo hii pamehifadhiwa na watu mbalimbali hufika hapa na kujionea baadhi ya vitu ambavyo Living Stone aliacha.

Ukarimu ni sehemu pekee ya wakazi wa mkoa huu hakika ukifika katiika mkoa huu utapata kujionea ni jinsi gani ni wakarimu na wanavyo ishi kwa kujariana kwa mambo yanayo ihusu jamii ya kigoma.

Uchapa kazi ndiyo sifa kuu ya wakazi wa mkoa huu ikiwa ni wakiume,wakike na hata wato ni watu wanaopenda kujishughulisha katika majukumu mbalimbali lengo ikiwa ni kujipatia kipato cha kujiendeshea maisha yao.

Asili ni moja ya kitu kinacho zingatiwa na hususa ni lugha hakika ukifika hapa utaweza kuzungumza lugha ya kiha tena kwa siku chache kama ilivyo kuwa kwangu tena ni rugha nyepesi sana ambayo ukijua utaweza kuongea na watu wa aina tofautitofauti wa kibantu mfano. 
Wakongomani,Wanyarwanda,Wahangaza,Warundi pamoja na Wahaya lakini pia Waganda.

Uasili wa vyakula bado uppo mpaka mjini huku unapata ugali wa mhogo pamoja na mafuta ya asili aina ya mawese ambayo hayajachanganywa na kemikali zozote ambayo pia inasemekana ni Dawa ya macho kwa wale wenye uoni hafifu mimi nimesha tumia nimeamini nikweli mafuta haya ni dawa.

Mawese ni mafuta ya kupikia ambayo yanatokana na mumea aina ya mchikichi ambapo hukamuliwa matunda yake yakiwa yamekomaa na kuzalisha mafuta hayo.

Wakazi wa mkoa huu wanapenda sana kula Samaki kuliko Nyama kwasababu samaki wanapatikana kwa wingi na huku wengine wakiamini kuwa samaki wazuri katika kujenga mwili kuliko Nyama.

Uwanja wa ndege ni moja wapo ya sehemu ambayo watu wengi huitumia kwenda sehemu mbalimbali kwa haraka kwamfano mikoa mingingine kama Dar es salaam ,Mwanza,Mpanda,Arusha n.k lakini pia nchi za nje kama DUBAI ambapo wafanya biashara hutumia uwanja huu kupokea mizigo yao.

Mkoa wa kigoma kwa sasa barabara nyingi za mjini pamoja na zinazo unganisha wilaya lakini pia mikoa baadhi yake tayari zimekwisha jengwa kwa kiwango cha lami jambo linalo warahisishia wakazi kutoka sehem moja kwenda nyingine.

Gari moshi ni mkombozi kwa wakazi wa kigoma pamoja na nchi jirani kama Burundi na Kongo ambapo watu hawa husafiri na kusafirisha mizigo kupitia reli ya kati kwa urahisi na gharama nafuu.

Wilaya ya Uvinza imejizolea umaarufu kwa kuwa na viwanda vingi vya kuzalishia chumvi ambapo pia viwanda hivyo vimebeba ajira za vijana wengi kutoka ndani na nje ya mkoa wa kigoma.

Lakini pia wilaya hiyohiyo  inasifika kwa kuzalisha samaki wazuri kutoka mto Malagalasi lakini pia kuzalisha ugari wa lowe utokanao na zao la mihogo vitu ambavyo hupendwa zaidi na wakazi wa mkoa huu pamoja na wageni.

Wilaya ya kasulu imejizolea umaarufu kwa kuwa na wawekezaji wengi hususa ni wafanya biashara ambao wameifanya kuwa mji wa kibiashara ukilinganisha na manispaa ya kigoma ujiji.

Kasulu ni wilaya ambayo pia wanazalisha zao la tangawizi kwa wingi ambapo ni zao la kibiashara hivyo watu kutoka mikoa balimbali huja wilayani humu ili kujipatia zao hilo na kwenda kuuza sehemu mbalimbali.

Vilevile kasulu kutokana na kuwa wilaya ambayo iko mpakani ndiyo wilaya inayopokea wakimbizi kutoka nchini Kongo na Bundi ambao wapo katika makambi ya Nduta na Mtabila wakiwa chini ya uangalizi wa serikili ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na hirika la kuhudumia wakimbizi duniani UNHCR.

Mkoa wa kigoma umejaaliwa kuwa na maeneo mengi sana yenye majini yanayo anza na herufi K jamboambalo hufurahisha pale mgeni anapo fika mkoani humo na kutamburiwa na bbadhi ya maeneo hayo ni haya yafuatayo
vKamala
vKibirizi
vKakonko
vKibondo
vKinazi
vKasulu
vKahabwa
vKalenge
vKasaka
vKatubuka
vKaseke n.k

Nazaleti ni moja ya sehemu ambayo wageni wengi hushangaa pale wanapo ambiwa kuwa kuna sehemu inaitwa nazaleti hivyo watu wengi hupenda kutembelea soko la nazaleti ikiwemo kununua vitu mbali mbali sokoni hapo.

Manispaa ya kigoma ujiji imejaaliwa kuwa na masoko mengi kwa mfano Mwanga senta, Buzebazeba,Kigoma marketi,Gungu namengineyo ambapo watu wengi hupata mahitaji yao mhimu ya majumbani.

Ujijipia ni eneo la ki historia ambapo inasadikika kuwa Dr. Living Stoni aliwahi kuishi lakini pia eneo hilo limehifadhiwa kisheria hivyo watali hufika pale na kujionea manzali iliyopo.

Mawenin ndiyo hospitali ya mkoa ambayo huhudumia wagonjwa wengi kutoka ndani ya manspaa lakini pia wilaya zingine za mkoa huo huku hospitali ya Baptst ikiwa inaendeshwa na serikali hvyo hupokea wagonjwa mbalimbali na wanapo zidiwa huhamishiwa maweni.

Jamanie kwa leo tuishie hapo ila kumbuka kuwa haya ni baadhi ya mambo kati ya mengi yanayo patikana hukoo mkani kigoma nilipata muda wa kufika mkoani hapo na kupita mtaa hadi mtaa ili kujua kigoma kunani nikaona si vyema nikajua pekeyangu nikaona nikushirikise nawewe msomaji wangu.

Nikushukuru kwa kuchukua muda wako kusoma makala hiifupi lakini pia kama kuna lolote unaweza ukanitafuta kwa mawasiliano yaliyop hapo chini na mimi sito sita kukujibu.
Namba.  +255 713 305 650
Facebook. MC GOODLUCK
Email.  Goodluckmc999@gmail.com




Chapisha Maoni

0 Maoni