Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

LAANA YA BABA,EPSODE-04

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER,
TULIISHIA HAPA
……..nasema tulia na kama ukijaribu kupiga kelele nakuchoma kisu cha tumbo na kisha nijimalize namimi alisema kijana huyo.
#EPSODE-04
Kwa kitendo hicho Anitha alikosa namna ya kujinasua ilimbidi kukubaliana na tendo lile ikizingatiwa kuwa tayari walikua na mapenzi ya siri tangiapo shuleni  wakayaanza misha ya ndoa kwa namna hiyo.
Maisha mkoani Dodoma yaliendelea huku binti akaendelea kudanganya anasoma na kuendelea kuomba pesa za ada na matumizi madogo madogo pesa ambazo zilitumika kumsomesha mume wake pamoja na kula huku wazazi hawana taarifa yakuwa mtoto wao aliolewa zaidi walijipa moyo anasoma.
Miezi kadhaa baadae Agness nae aliolewa katika kijiji cha kazulamimba mkoani kigoma ambapo nae wazazi waliibariki ndoa hiyo basi aliishi kwaamani na mume wake kama ilivyo kwa dada yake Vanesa  alie olewa Morogoro.
Wazazi walifurahi sana kuona mabinti zao wawili kwenda kuanzisha familia pamoja na kukuza ukoo jambo lililo wapa nguvu kundelea kutuma pesa kwa Anitha kwani hawakujua kama Anitha amekwisha kuolewa .
Mwaka mmoja baadae Anitha alijifungua mtoto na wazazi wake hawakupata taarifa yeyote juu ya jambo hilo zaidi waliendelea kutuma pesa kwaajili ya matumizi kwa imani kuwa yupo Mwanza kimasomo kumbe yuko Dodoma kindoa.
Basi siku hazingandi kijana aliingia mwaka wapili akiwa na furaha kubwa kwa kuwa na mtoto pamoja na mke ambae anamuwezesha kusoma na mapenzi yaliendelea kushamiri huku wakiwe wamekwisha kusahau yaliyo kwisha kutokea kipindi cha nyuma kwani binti Anitha aliyapenda maisha yale.
Kijana alikaachini na kuona kuwa kuna haja ya kwenda kujitamburisha kwa wazazi wa Anitha lakini ilimuwea vigumu akaona amshirikishe amitha lakini iliwachukua muda kufikia mwafaka ya namna gani atafika kwa wazazi.
Basi mwafaka walio fikia ikaonekana kuwa kijana arudi pekeyake akawaeleze wazazi na baadae wataenda wote mara baada ya kijana kujulikana nyumbani kwa wazazi wa anitha,Mara safari ya kijana ilianza kutoka Dodoma kuelekea katika kijiji cha katete Mkoani Kigoma.

Itaendelea……
N.B: Majina ya wahusika katika simulizi hii yemehifadhiwa kwasababu za kiusalama kwasababu hili ni tukio la kweli ambalo lilitokea miaka kadhaa iliyo pita hivyo nimeona si vyema kutumia majina harisi ya wahusika kwa hilo nitaomba radhi msomaji wangu.
KWA MAHITAJI YA NAKALA YA SIMULIZI HII WASILIANA NA KITENGO CHA MASOKO KUPITIA:
+255 713 305 650

KUPATA STORI,HABARI,ELIMU,BURUDANI NA DINI TEMBELEA MITANDAO YETU IFUATAYO:
BLOG.planmediatz.blogspot.com
Facebook.PMTV_TZ
YouTube.PMTV_TZ
Instagram.pmtv_tz
Twitter.channel_plan

PLANMEDIA©2018


Chapisha Maoni

0 Maoni