Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

HILI NDILO NENO LA RITHA KWA WADAU WA MUZIKI

NA,GOODLUCK CHRISTOPHER
Muimbaji wa nyhimbo za kumsifu Mungu /injili Tanzania anaefahamika wajina la Ritha Komba amesema hajawahi kuwa kimya bali anaendelea kuandaa kazi mpya, ameyasema mapema leo wakati akizungumza na PLAN MEDIA TV.

Ritha ameieleza PLAN MEDIA TV Kuwa kwasasa anaendelea kutengeneza video mpya unao itwa Nguvu yangu kwaajili ya kukamilisha albam yake mpya inayo enda kwa jina la Rafiki inayo tarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni lakini kabla zindua albam hiyo ataachia video na audio ya Nguvu yangu.

Muimbaji huyo ametoa neon kwa wadau wa muziki wa njili ndani na nje ya Tanzania kutoa kipaumbele kwa waimbaji  na kutafuta namna ya kutoa nafasi kwa waimbaji kufikisha nyimbo hizo kwa mashabiki ili kulifikisha neon kwa mataifa.


Ritha amemaliza kwa kuomba ushirikiano kutoka kwa mashabiki wa muziki wa injili,maombi pamoja na maoni kutoka kwao ili aifanye kazi ya Mungu.

Chapisha Maoni

0 Maoni