Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

LAANA YA BABA,EPSODE-5

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER,
TULIISHIA HAPA
Mara safari ya kijana ilianza kutoka Dodoma kuelekea katika kijiji cha katete Mkoani Kigoma.
EPSODE-05
…… Mara safari ya kijana ilianza kutoka Dodoma kuelekea katika kijiji cha katete Mkoani Kigoma.
Kijana akafika kijijini akamtafuta mzee mwenye busara kwaajiri ya kwenda nyumbani kwa wazazi wa  Anitha, basi mzee yule alifika nyumbani kwa wazazizi wa anitha kwaajiri ya kuwajuza ujio wa kijana huyo.
Mze huyo alipokelewa vyema nyumbani hapo kama mgeni japo wazazi wa Anitha hawakujua  kilicho mpeleka nyumbani hapo basi alijitamburisha na kujieleza kuwa ;kuna jambo kubwa limempeleka nyumbani hapo.
Wazazi wa anitha wakawa wanashauku kubwa yakujua ni jambo gani lilikua limemleta mzee huyo “Wazazi wenzangu kubwa zaidi lilonileta hapa ni jambo la kufurahisha sana kwani nimekuja kuwajulisha kuwa kijana wangu amemchukua kijana wenu na anaishi nae kama mke na mume yapata miaka miwili tangu waoane na cha kufurahisha zaidi wamebahatika kupata mtoto wakiume hivi karibuni alisema mzee huyo.
Wazazi wa anitha wakaanza kushangaa na kutahamaki wa kumuuliza mzee huyo ili kujua ni kijana yupi anamzungumzia kwakua wezee hao wanawatoto wakike wapatao wawili ambao wamekwisha olewa, mzee ni mtoto gani huyo? Waliuliza wa Anitha.
Basi mzee huyo alionesha tabasamu usoni mwake na kutaja Anitha, Anitha? Waliuliza wazazi wa Anitha, Ndiyo Anitha alijibu kwa kujiamini mzee Yule, Mbona mtoto wetu anasoma waliongea wazazi wa Anitha.
Nikweli kabisa wakati wanatoka hapa kijijini hawakuweka wazi kama wanaenda kuoana lakini ukweli tokea siku zile yapata mika miwili wakiishi kama mke na mume na siyo kusoma kama mnavyo dhani aliongea mzee yule.
Wemzee mbona unanivuruga lakini ebu ongea mambo ya maana na si kuongea utani saizi aliongea Baba wa Anitha, Si muda wa kutaniana mzee mwenzangu na hivi kijana amenituma kuja kuomba nafasi ili kesho aje kujitamburisha aliongea mzee Yule.
Basi babayake na ndipo alimrarua ngumi za uso akadondoka chini watu wakawahi kuja kuamua ugomvi ulie na kumuamlisha Yule mzee kwamba aondoke na badala yake kijana mwenyewe aje wapate kuzungumza wote huku akiwa na jaziba ya kufa mtu.
Mzee Yule aliamua kuondoka huku akiwa na maumivu makari kutokana  na kipigo alicho kipokea kutoka baba Anitha alijikongoja mpaka kufika kwake kwani alikua hana jinsi ya kufanya.
Ikawa mzee alipo fika aliaamua kumweleza kijana kilicho mkuta huko ndiupo kijana aliogopa sana kwamba endapo ataonekana mbele ya baba Anitha kichwa chake kitakua harari yake.
Kijana hakutaka kuchelewesha mambo alikusanya kila kilicho chake na usiku wa manane aliamua kutoroka na kuamua kurudi huko Dodoma huku akiwa na woga mkubwa kwamba endapo akikutana na baba Anitha basi atakua amekwisha.
Wki moja baadae baba Anitha alipokea taarifa kuwa kijana amekwisha kutoroka pasipo kuzungumza nae wala kumuona hivyo alipatwa na gadhabu juu ya kijana Yule lakini alikua hana la kufanya kwa muda huo.
Basi kijana alikua amekwisha kurudi kwa mke wake huko Doma akamweleza kilicho jiri huko basi  Anitha alipatwa na hofu kubwa moyo na kuwaza kwamba atarudi viupi nyumbani kwao.
Lakini pia kwa kijana huo ndio ulikua mwisho wa masomo yake kwani alikua hana uwezo wa kujilipia ada ya mwaka mmoja uliokua umebaki maana alikua anategemea mfuko wamkwewe.
Masha yakaanza kuwa magumu kiasi cha kukosa chakula ikizingatiwa hawana kazi yeyote mjini inayo waingizia pesa basi wakaji change change na miezi kadha baadae walifungasha vilago mpaka kijini kwao katete lakini wakafikia nyumbani kwa wazazi wa kijana.
Wakati wakiendelea kutafakari ni jinsi gani wanaweza kwenda kuomba msamaha kwa wazazi wa Anitha basi baba anitha alikua amekwisha kupata taarifa kuwa wapo kijijini hapo.
Wiki kama mbili baadae alifanya upelelezina kujua wapi walipondipo alipo muagiza mjumbe na kuwataka siku mbili baadae waweze kufika  nyumbani atakua na mazungumzo nao.
Mjumbe Yule alipata kufikisha taarifa ile lakini wao hawakuweza kutii wito ule na badala yake waliamua kuto kwenda wakihofia kwamba  huenda akawadhuru.

Baba Anitha alichukia sana na zilipo pita wiki mbili na nusu alimwagiza mjumbe wapili  lakini bado pia hawkuitika wito basi aliwachoka watoto wale.
Ikapita siku moja ndipo aliamua kuchukua uamzi mgumu wa kuandika kwenye kaeatasi maneno yafuatayo “Katika mabinti zangu watatu ambao ni Anitha,Agness na Vanesa kuanzia leo watafanikiwa mpaka washangae watoto wafuatao Agness na Vanesa lakini namlaani mtotowangu nilemzaa Anitha pamoja na mmewake kuanzia leo hawatokaa wafanikiwe kwa lolote mpaka kufakwake isipo kuwa watakapo kuja kuniomba msamaha na kiasi cha pesa kisicho pungua milioni4 za kitanzania pamoja na mbuzi mmoja  nje na hapo hawato fanikiwa daima na milele.“
Basi baada ya kuandika wakala huo  akamuagiza mjumbe wa tatu aweze kuwapelekea nae hakusita aliwafikishia Anitha alilia sana na kujutia alicho kifanya lakini wahenga husema majuto ni mjukuu na maji yakisha mwagika haya zoeleki tena.
Paka leo hii Anitha anaishi maisha mabaya sana istoshe hana uwezo wa kupata kiasi cha milioni 4 na istoshe hana kazi yeyote na Yule kijana ni kama wametengana kutokana na ugumu wa maisha ikizingatiwa mtoto wao anahitaji matunzo.
Nahuu ndio mwisho wa simulizi yetu hatimae Anitha ameishia kulaaniwa  kwa mambo aliyo jitakia kupitia simulizi hii basi tupate kujifunza kitu.

USIKOSE SIMULIZI ZINGINE NZ NZURI ZINAZO KUJIA HIVI KARIBUNI KUPITIA HAPA HAPA PLAN MEDIA.

MWISHO

N.B: Majina ya wahusika katika simulizi hii yemehifadhiwa kwasababu za kiusalama kwasababu hili ni tukio la kweli ambalo lilitokea miaka kadhaa iliyo pita hivyo nimeona si vyema kutumia majina harisi ya wahusika kwa hilo nitaomba radhi msomaji wangu.
KWA MAHITAJI YA NAKALA YA SIMULIZI HII WASILIANA NA KITENGO CHA MASOKO KUPITIA:
+255 713 305 650

KUPATA STORI,HABARI,ELIMU,BURUDANI NA DINI TEMBELEA MITANDAO YETU IFUATAYO:
BLOG.planmediatz.blogspot.com
Facebook.PMTV_TZ
YouTube.PMTV_TZ
Instagram.pmtv_tz
Twitter.channel_plan

PLANMEDIA©2018



Chapisha Maoni

0 Maoni