Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

NDOA ZA UTOTONI

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Kwa mara nyingine tena plan media inakuletea makala yenye mafundisho ya hali ya juu lengo likiwa ni kila mtanzania kupata elimu juu ya mabo ambayo hayajui na kama anayajua basi tunamuongezea maarifa chamsingi ni kuhakikisha hupitwi na kitu kwa kutembelea planmediatz.blogspot.com kila siku.

Na makala ya siku ya leo tumeamua kuwaletea suala nyeti sana ambalo watu wengi hawalielewi kiundani hivyo pasipo kupoteza muda niovyema nika kukaribisha kuchukua muda wako kusoma makala hii kwa umakini na Kama kuna sehemu huelewi basi uta uliza kwa kukoment hapo chini.
Swali linalo gonga vichwa vya watu ni je mimba za utototoni ni nini? 

Kiukweli hapa kila mtu anajibu lak analo lifikilia kutokana na uelewawaalio nao ili ni jambo lisilo pingika kwamba mimba za utotoni ni ule ujauzito unaopatikana kwa mtoto wakike akiwa chini ya umri wa miaka 18.
Kwa mjibu wa taasisi na mashirika mengi duniani yanayo tetea haki za watoto mimba za utotoni zinapigwa vita na watetezi hao kwa dhana kwamba ni noja wapo ya unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto nah ii ni ukweli kwamba suala hili ni ukweli usio pingika kwamba ni ukatili wa hali ya juu kwa mtoto chini ya umri wa miaka 18.

Daaaah!!! Swali ambalo huwa najuliza na likawa linaniumiza kichwa ni je, ni kwani mimba za utotoni zinatokea jeee? Hapo nilikua nawaza kwa sauti na wala sikupata jibu, baada ya kukosa jibu unajua nilifanya kitu gani? Hahahaha!!! Ebu angalia nilicho kifanya.

Aiseeeeee! Nimegundua utafiti ni kitu kizuri sana na ndo maana napenda sana kufanya utafiti basi msomaji wangu niliamua  kupita mta kwa mtaa nikihoji lengo nikitaka kujua kwanini mimba za utotoni zinatokea? Basi mtaani ilikua hivi:
Ø Utandawazi
Ø Tamaa za watoto wenyewe
Ø Malezi
Ø Mila na Tamaduni
Ø Umasikini

Na hivyo ndivyo ilivyokua mtaani watu waliweza kufunguka vile vyenye wanaelewa lakini si kuishia hapo niliamua kuhoji kwa kina kujua  vitu hivyo vinasabisha je hizo mimba unajua ilikuaje? Usijali nilifuatilia kwa kina ikawa hivi:

UTANDAWAZI
Basi neon hili lina maana nyingi kama nini mimi nikaamua kuchukua neon hili mabadiliko katika Nyanja mbalimbali katika maisha ya kibinadamu kwamfano mawasiliano nimetumia mfano huu lakini kuna vingi vinavyo fanana na hilo.

Utandawazi ni kitu ambacho kinachangia watoto kujihusisha na na mitandao ya kigono kingali wadogo na wanapo jaribu tu kujiingiza katika tendo lisilo takatifu la ndo hujikuta wamezama na matokeo yake huwa ni kuambulia kubeba ujauzito chini ya umri wa miaka 18.

TAMAA ZA WATOTO WENYEWE
Uuuuuuuuuuuwi!! Hapa sasa nilipata utata ila nilipata kuchagua jibu moja kati ya mengi nalo ni baadhi ya vijana wanaonekana kutomani vitu wasivyo navyo ili kukidhi mahitaji yao madogomadogo ambayo hawayapati katika familia zao mfano. Zawadi ndogondogo kutoka kwa mwanaume kama chips mayai, kutolewa out yani katika maeneo ya starehe, Lifuti, Simu na vocha zake na vitu vingine kama hivyo.

Basi iko hivi sikuzote ukila utaliwa kimsingi iko hivyo na siku zote wahenga husema tama mbaya hivyo matunda ya kutamani huwa ni kuambuliamatatizo kwa mantiki hiyo basi mabinti wengi hujikuta wakitumbukia kwenye dimbwi la mimba kingali watoto.

MALEZI
Malezi ni suala pan asana hivyo wakati nikipita mtaa mpaka mtaa nilipata kupewa maana nyingi za neon hilo ila kwa leo naomba tutumie hii hapa. Ni yale mafundisho na maonyo ambayo mtoto hupewa kutoka kwa wazazi ama walezi wa mtoto huyo.

Basi wahenga husema mtoto umleanyo ndivyo akuavyo kwa mantiki hii wazazi wengi wamekua wakilia watoto wao vibaya ikiwemo kuwapa uhuru ulio pitiliza jambo linalo wafanya watoto wengine kuwa na tabia mbaya ambayo hupelekea watoto wengi kujisahau na kujiingiza katika dimbwi la mahusiano ya kingono kingali wadogo hali inayo pelekea kubeba ujauzito chini ya umri wa miaka 18.

MILA AU TAMADUNI
Haya ni masuala ya mambo yanayo fanya na asili moja ya watu wanao fanana kwamfano ukoo,kabira au inaweza kuwa hata taifa hivyo mambo haya huchangia mimba za utotoni katika baadhi ya makabira katika nchi yetu ya Tanzania au bara la Afrika kwa ujumla.

Kwa baadhi ya makabira mfano wasukuma,wakurya,wamaasai nawewengine kama hao kwa kipindi cha nyuma waliongoza sana katika mimba hizo za utotoni richa ya serikali na wadau mbalimbali kupiga vita sula hili kwani wao waliamini kumuozesha binti mapema huongeza heshima ya ukoo wao pamoja na kujipatia mifugo kutoka kwa muoaji.

UMASIKINI
Niile hali ya binadamu kukosa mahitaji mhimu ambayo binadamu anastahili kupata kwamfano pesa,chakula,mavazi pamoja na malazi na vitu vingine kama hivyo hii ndiyo dhanaya umasikini na mtu anapo kosa vitu hivyo basi anapaswa kuitwa masikini.

Nikweli kabisa kwamba binadamu ili akamilike lazima apatemahitaji yake yamhimu hivyo basi kwa mtoto wa lkike anapo kua amekosa mahitaji yake nyumbani basi huamua kutafuta ama kuombaomba kwa wanaume ili kukidhi haja zake kwa Kiswahili cha vijana waleo wanasema kudanga  jambo ambalo huwapelekea kubeba ujauzito kwasababu hukosa vya kuwalipa walio wapatia vitu hivyo na kuamua kulipa utu wao.

Jamanie hayo ni baadhi ya ambayo nimeyapata huku mitaani ama uswazi uswahilini kusema kweli uswahilini kuna vituko ten asana lakini swali la kujiuliza mimi nawewe ni je suruhilo la hili ni lipi? Usijali bado nipo huku uswahilini pengine ngoja niendelee kuhoji harafu tuchangie kitakacho patikana.

SURUHISHO.
Msomaji wangu kila chenye mwanzo hakikosi mwisho nimejaribu kuhoji sana na kupata majibu mengi na moja katka hayo ni haya hapa yafuatayo.
Ø Kutoa elimu ya jinsia kwa watoto
Ø Kuwa karibu na watoto wetu
Ø Matmizi bora ya utandawazi
Ø Kuridhika na kipato cha mzazi wako
Ø Kuacha nila na tamaduni potofu
Ø Kuacha tama
Ø Malezi bora kwa watoto

Hayo yalikua ni baadhi yamambo yanayo paswa kuzingatiwa zaidi ili kujiepusha na mimba za utotoni lakini ikumbukwe kuwa mimba za utotoni huharibu taifa kwani hukatisha ndoto ya mtoto jambo ambalo hupelekea kuwa na wanchi wajinga hivyo tuchukue tahadhali mapema kabla haya jatukuta.

Ebanaeee kutoka huku uswazi uswazini maarufu kama mtani kwetu kwa leo sinala ziada  hivyo sina budi kurudi mitamboni pale mitaa ya ilala bungoni kuwasirisha kile nilichokipata huku mtaani lakini pia tukutane kwenye makala nyingi sana zinazo kuja hivi karibuni naitwa GOODLUCK CHRISTOPHER Nitafute kwa mawasilianoyafuatayo
Facebook. MC GOODLUCK
Contact. +255713 305 650
         






Chapisha Maoni

0 Maoni