Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

LAANA YA BABA, EPSODE-03

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER,
TULIISHIA HAPA.
…………… hivyo wazazi walijikusanya na kumpatia pesa kwaajiri  ya kumpeleka shule.
#EPSODE-03
Baada ya wazazi kujikusanya walimkabidhi kiasi cha milioni moja za kitanzania ndipo walipanga safari binti akijua wanaelekea chuoni huko mwanza lakini haikuwa hivyo kwa mwanaume Yule na kwavile Anitha alikua hajui njia yakwenda huko mkoaniMwanza alimsikiliza mwanaume alikua anafuata njia anayopita mwanaume yule.
Wakapanda gari moshi kuelekea mkoani Dodoma kwa makubaliano yakuwameoana lakini mwanaume akiwa ameenda kusoma chuo cha St. Joseph tawi la Dodoma katika taaluma ya Ualimu wakati huo binti Anitha alikua hajui chochote kuhusu hilo kwani mwanaume Yule hakumdokeza maana alijua akimdokeza lengo lake halita kamilika.
Ikawa walipo fika Dodoma mwanaume akachukua ile pesa na kumweleza Anitha kuwa hawato weza kwenda mwanza na hawezi tena kusoma na badala yake pesa hiyo itatumika kumsomesha yeye na si Anita kama ilivyo tarajiwa.
Kutokana na ugeni wa mji lakini pia kuchukuliwa pesa na simu yake Anitha alichanganyikiwa na kwa muda huo hakujua ajiokoe vipi katika mazingira hayo hivyo siku nzima alikua ni kama mtu ambae hajitambui ilimbidi kuwa mpole huku akisubiria kitakacho endelea.
Ikafika usiku ndipo Anitha alishangaa kuona anapelekwa chumbani  kwaajili ya kulala huku akijua kuwa kijana atakua ametafuta chumba kingine cha kulala lakini haikuwa hivyo kijana alimuamru kulala kitanda kimoja na kumweleza wazi kuwa amemuoa.
……nisikilize Anitha sikuzote nimekua nikitafuta njia ya kuishi nawewe lakini nimekua sipati nafasi hiyo hivyo najua leo hii hauna ujanja utakua mke wangu kuanzia leo mpaka pale kifo kitakapo tutenganisha alisema kijana huyo.
Anitha alilia sana huku akitaka kutoroka chumbani pale lakini kijana alimshikia kisu na kutaka kumchoma……..nasema tulia na kama ukijaribu kupiga kelele nakuchoma kisu cha tumbo na kisha nijimalize namimi alisema kijana huyo.
Itaendelea……
N.B: Majina ya wahusika katika simulizi hii yemehifadhiwa kwasababu za kiusalama kwasababu hili ni tukio la kweli ambalo lilitokea miaka kadhaa iliyo pita hivyo nimeona si vyema kutumia majina harisi ya wahusika kwa hilo nitaomba radhi msomaji wangu.
KWA MAHITAJI YA NAKALA YA SIMULIZI HII WASILIANA NA KITENGO CHA MASOKO KUPITIA:
+255 713 305 650

KUPATA STORI,HABARI,ELIMU,BURUDANI NA DINI TEMBELEA MITANDAO YETU IFUATAYO:
BLOG.planmediatz.blogspot.com
Facebook.PMTV_TZ
YouTube.PMTV_TZ
Instagram.pmtv_tz
Twitter.channel_plan

PLANMEDIA©2018


Chapisha Maoni

0 Maoni