Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

BERKO ATOA FUNZO KWA WACHEZAJI CHIPUKIZI KUTOKATA TAMAA.


NA.PATSON MWITA.

MCHEZAJI wa timu ya Bombom Fc ya Ilala, Suleiman Mohammed anayefahamika kwa jina la Berko  anayecheza nafasi ya Golikipa namba moja wa timu hiyo,ambapo hadi sasa amedumu katika klabu hiyo kwa muda wa miaka tisa[9],alianza kupenda soka tangu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili[12],kabla ya kuwa golikipa alikuwa anacheza nafasi ya ushambuliaji lakini alivutiwa zaid na udakaji na golikipa wa yanga Yoberko wakati huo akiwa mchezaji wa yanga.

 Suleiman ambaye amewahi kuwa mshindi wa tuzo ya mashindano ya JK yaliyofanyika mwaka jana na kufanya kuibuka golikipa bora wa mashindano hayo,Bombom ilimfanya qweze kushiriki mashindano mbalimbali kama vile COPA coca cola,JK inasifika kuibua vipaji kama vile Ramadhani sigano kwa sasa anachezea Azam fc,Ibrahim ajibu anachezea timu ya yanga na Hassan isiaka anayekipaga timu ya mtibwa sugar.

 Akielezea mambo asiyoweza kuyasahau Suleimani alisema’’sitosahau  niliposhindwa kufuzu kucheza timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka kumi na saba 17[Serengeti boys];jambo lingine ambalo sitoweza kusahau niliposhindwa kucheza soka kwa kipindi cha miezi hisiyopungua miwili’’.hayo yamesemwa na Suleiman.


Timu aliyoifurahia katika maisha yake ya soka  ni Bombom Fc anayoitumikia mpaka sasa,vile ilimpaumaharufuna mafanikio alioyapata katika maisha yake ya soka;pia ametoa ushauli kwa wachezaji chipukizi ambao wamekata tama kwenye soka na kuwaomba wasikate tama na badala yake wafanye mazoezi ya kutosha  ili wafikie malengo yao kwenye soka.


[PICHANI NI GOLIKIPA WA BOMBOM FC SULEIMAN BERKO {KATIKATI}AKIWA NA WACHEZAJI WENZAKE.PICHA NA MAKTABA].

Chapisha Maoni

0 Maoni