[PICHANI MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA,ALIYEVAA SHATI JEUPE AKIWA SAMBAMBA NA JESHI LA POLISI.]PICHA NA MAKTABA.
KILIMANJARO.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo amekabidhi
gari 26 za polisi mkoani Kilimanjaro zilizopelekwa kwa ukarabati,ambapo gari
hizo zimefanyiwa majaribio leo na zipo tayari safirishwa hadi Daresalaam kwa
ajili ya matumizi ya kiusalama,mbali na kufanyiwa ukarabati gari hizo
zimefungwa kamera maalumu zitakazo saidia jeshi la polisi kupata ushaidi Zaidi.
Wakati akiongea na moja ya chombo cha habari kilichopo hapa nchini,amesema anataka kuifanya Daresalaam kuwa jiji la kisasa na mfano kwa miji mingine,pia ameelezea juu ya mpango wa kufunga kamera katika vituo vyote vya mkoa huo ili kurahisisha shughuli za kiuchunguzi, ambapo OCD , kanda maalumu, pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi wataweza kuona kile ambacho kinafanyika.
Wakati akiongea na moja ya chombo cha habari kilichopo hapa nchini,amesema anataka kuifanya Daresalaam kuwa jiji la kisasa na mfano kwa miji mingine,pia ameelezea juu ya mpango wa kufunga kamera katika vituo vyote vya mkoa huo ili kurahisisha shughuli za kiuchunguzi, ambapo OCD , kanda maalumu, pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi wataweza kuona kile ambacho kinafanyika.
Kazi kubwa ya gari hizo ni kupambana na uhalifu kwa kasi
kubwa na kuweza kuwafikia wahalifu popote walipo pasipo na vikwazo,ambapo gari
hizo zilizofungwa kamera zitakuwa
suruhisho kwa uhalifu jijini Dar es salaam na kupunguza ujambazi mkoani humo.


0 Maoni