Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

ARSENAL YAMPA TIKETI RONALD KOEMAN.

                                        
 .LONDON.

Everton imemfungashia virago Ronald Koeman baada ya kupokea kichapo cha mabao 5-2 siku ya jumapili kutoka  kwa washika bunduki wa London Arsenal,Taarifa kutoka kwenye uongozi wa klabu hiyo inasema "ingependa kutoa shukrani kwa Ronald Koeman kwa huduma aliyoitoa klabuni hapo kwa miezi 16 iliyopita".ambapo msimu wa ligi wa mwaka 2017/2018 everton imeshinda michezo miwili pekee.

"Bado ninaamini ninaweza kubadilisha hali yote," Koeman alisema hayo kwenye mahojiano kabla ya mchezo wuliofanyika Jumapili,Koeman anakuwa kocha wa tatu kutimuliwa kwenye klabu za uingereza msimu baada ya Frank de Boer timu yake ilipofungwa na Crystal Palace na Craig Shakespeare timu yake ilipofungwa  na Leicester City.MDutchman HUYO mwenye umri wa miaka 54, ambaye ameiongoza Everton hadi nafasi ya saba katika msimu wa ligi uliopita licha ya kiasi cha pesa walichokitumia kufanyia usajili ambapo  Everton ilitumia kiasi cha  £ 140m wakati wa majira ya joto.

Mmiliki wa Everton Farhad Moshiri alimpa tumaini Koeman wiki mbili zilizopita baada ya kushinda kwao 1-0  dhidi ya Burnley, lakini baada ya hapo walikutana na timu ya Brighton na walipoteza pia ilipoteza na  Lyon, katika Europa League, kabla ya kuadhibiwa na Arsenal 5-2 kwenye uwanja wa Goodison Parkl.

Siku ya Jumapili Koeman aliandika kuwa kupata matokeo dhidi ya Arsenal ilikuwa "haiwezekani" baada ya mchezaji wao kutolewa uwanjani na kufanya Everton kucheza pungufu wakiwa 10 uwanjani wakati huo likuwa 2-1.Huku nafasi ya  Everton kufufuzu kwenye Europa League  ni ndogo, ambapo ipo mwisho kwenye msimamo wa kundi hilo linalo zihusisha klabu za  Merseysiders ,Atalanta,Lyon na Apollon Limassol.


Mchezaji wa zamani wa Leicester City Steve Claridge, akizungumza kwenye BBC Radio 5 aliiambia kuwa baada ya kupoteza kwa Everton siku ya Jumapili,"kunatakiwa kufanyike mabadiliko ya haraka  "Kwa ushahidi huu, Everton ipo katika shida kubwa," alisemahuko Everton,pia ameishauri timu hiyo ifanye usajili wa kutosha january mwakani ili kuiimarisha klabu.

Chapisha Maoni

0 Maoni