Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

 UCHAGUZI WA MARUDIO WAAIHIRISHWA MAGHARIBI MWA KENYA
Watu wawili wameuawa kwa kupigwa risasi wakati wa makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa upinzani katika maeneo hayo.
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati amesema tume imechukua hatua hiyo baada ya upigaji kura kutatizwa na ukosefu wa usalama.
Katika majimbo hayo ya Kisumu, Siaya, Migori na Homa Bay, wafuasi wa upinzani walifunga barabara za kuelekea katika vituo vya kupigia kura na kukabiliana na maafisa wa polisi siku yote.
Katika baadhi ya maeneo, makarani na maafisa wengine wa kupigia kura hawakufika vituoni kutokana na kile mmoja wa wasimamizi alisema ni kuhofia usalama wao.
Serikali ilikuwa imewatuma maafisa wa polisi katika maeneo mbalimbali kushika doria.
Gavana wa jimbo la Kisumu Prof Anyang' Nyongo amewatuhumu polisi kwa kutumia "magenge ya watu" kuwashambulia wafuasi wa upinzani.
Ameambia BBC kwamba watu wawili wamefariki eneo lake na wengine 29 wanauguza majeraha.
Prof Nyong'o amesema hawataruhusu uchaguzi wa marudio ufanyike katika kaunti hiyo.
"Nimetangaza kama gavana wa hii kaunti wiki moja ya maombolezi ambapo wakati huo hakutakuwa na sherehe. Kwetu uchaguzi huwa ni sherehe," amesema.
Amesema iwapo tume hiyo itaendelea kusisitiza uchaguzi ufanyike, basi wataenda kortini kutaka uzuiwe.

SOURCE. BBCSWAHILI.COM

Chapisha Maoni

0 Maoni