Akaunti ya
mtandao wa Twitter ya rais Donald Trump ilipotea kwa muda siku ya Alhamisi
lakini, ikarudishwa baadaye , kampuni hiyo imesema.
Twitter imesema kuwa akaunti hiyo kwa jina @realdonaldtrump iliondolewa
na mfanyikazi mmoja na baadaye kuelezea kuwa ilikuwa siku yake ya mwisho kazi.
Akaunti hiyo iliondolewa kwa muda wa dakika 11 na sasa kampuni
ya Twitter inachunguza.
Bwana Trump ambaye ni mtumizi wa mtandao wa Twitter wa mara kwa
mara akiwa na wafuasi milioni 41.7 hajatoa tamko lolote kuhusu swala hilo.
Siku ya Alhamisi jioni, wale waliotembelea akaunti ya rais Trump
waliona ujumbe uliosema ''pole ukurasa huu hauko kwa sasa!''
Baada ya akaunti kurejeshwa , ujumbe wa kwanza wa bwana Trump
ulikuwa kuhusu ule mpango wa Republican wa kupunguza kodi.
Twitter imesema kuwa inachunguza tatizo hilo na kuchukua hatua
za kuhakikisha kuwa kisa kama hicho hakitokei tena.
Kampuni hiyo ilisema katika ujumbe wake kwamba wamebaini katika
uchunguzi wao kwamba kisa hicho kilifanywa na mfanyikazi anayewahudumia wateja
ambaye alifanya hivyo katika siku yake ya mwisho ya kazi.
Tunatathmini kisa chote kikamilifu.
Bwana trump alijiunga na mtandao wa twitter mnamo mwezi Machi
2009.
Amekuwa mtumiaji mkubwa wa mtandao huo kwa kukuza sera zake
mbali na kuwashambulia wapinzani wake wakati wa kampeni za urais 2016 na hata
baada ya kuchukua mamlaka mnamo mwezi Januari.
SOURCE. BBCSWAHILI.COM


0 Maoni