Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

BETHA AZUNGUMZIA UJIO WA ALBAM YAKE MPYA

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Mujimbaji wa nyimbo za injili  Tanzania anae fanya vizuri kwa sasa  Betha Mwafilombe amezungumzia ujio  wa albam yake mpya ya kwa neema tu kuwa imepokelewa vyema na wadau wa muziki wa ijnili hapa Tanzania zaidi ya alivyo dhania kuwa itapokelewa hivyo.

Aidha  Betha  amesema kuwa albam hiyo yenye nymbo nane inafanya vizuri sana kwasasa katika ulimwengu wa injili hapa nchini huku albam hiyo ikichezwa na vituo vingi vya radio na wasikilizaji wa radio hizo wameonesha kuzipenda nyimbo hizo.

Vilevile  Betha hajapata msambazaji wa kuisambaza albam hiyo ili iwafikie watu wa mikoa ya mbali na mkoa wa Dar es salaam hivyo anahitaji msambazaji wa kuweza kuisambaza albam hiyo maana anatamani ifike kila kona na kila anae ihitaji aipate.

Albam hiyo inapatikana kwa kiasi cha Tsh. 5000/= Tuu. Mtu ane ihitaji kwasasa anakuletea mwenyewe mali ulipo kupitia mawasiliano nitakayo kuwekea hapo chini na wale wa mikoani amesema kuwa anawaagizia kwa njia ya mabasi na inakufikia popote ulipo.

Pia Betha amesema yuko tayari kwa mialiko na yupo tayari kutumika mahali popote kwa utukufu wa Mungu hivyo kwa watu wa mikoani na nje ya nchi wawe huru kumualika makanisani, mikutano na matamasha hato sita kufika kwa utukufu wa Bwana.

Betha amesema kuwa uzinduzi wa albam hii utafanyika viwanja vya Mababu CCM wilaya ya Kyera mkoani Mbeya tarehe 7/7/2018 amewaomba wadau wa mziki wa injili kujitokeza kwa wingi siku hiyo.

Hata hivyo betha amemaliza kwa kusema kuwa video ya albam hiyo inatarajiwa kufanyika mwaka u8jao wa 2018, hivyo wadau na wasio wadau wa muziki wa injili wajipange kuipokea video nzuri na yenye ubora wa hali ya juu mapema hapo mwakani.

MAWASIILIANO YA BETHA
 HOTLINE: 0767 406 265
INSTAGRAM: BETHA J MWAFILOMBE
FACEBOOK. BETHA J MWAFILOMBE


Chapisha Maoni

0 Maoni