Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

KILIO CHA WAFANYA KAZI WA NDANI TANZANIA

Na. goodluck christopher
Elimu ni kitu cha msingi sana katika maisha ya binadamu na vitabu vya Mungu pia vinasisitiza elimu kuwa ni jambo la kuzingatia sana maana katika karne hii ya 21 suala la elimu limekua ni lamsingi na la maana sana ikizingatiwa kuwa asilimia kubwa za vitu vina hitaji elimu hivyo suala hili halikwepeki kwa mtu yeyote.

Katika miaka kadhaa iliyo pita elimu ilikua haizingatiwi kwa kiasi kikubwa hususani vijijini na hasa kwa watoto wakike ambapo iliaminika kuwa watoto wakike ni wakubaki nyumbani huku wakisubiraa kuolewa jambo ambalo lilikua ni imani potofu na ukoefu wa elimu.

Mbali na elimu kutolewa juu ya hilo bado kuna jamii zinaendelea na imani hizo potofu ambazo zimepitwa na wakati huku jamii hizo zikiwa zinaamini kuwa ni sahihi kufanya hivyo na hasa katika maeneo ya vijijini.

Mpenzi msomaji wa Plan Media napenda kuku karibisha rasimi katika makala hii yenye mafundisho ya hali ya juu kuhusiana na wafanya kazi wa majumbani kwamaana ya wadada wanaofanya kazi za ndani [HOUSE GIRL].

Tunapo zungumzia wafanya kazi wa ndani ni watu/mtu ambae ameajiriwa kwaajili ya kusaidia ama kufanya kazi za nyumbani ili kujipatia kipato cha kujiendeshea maisha yake kama zilivyo kazi zingine ambazo watu huzifanya kwa ajili ya kujiendeshea maisha ya kila siku.

Kama mfanya kazi mwingine alivyo kua na haki  basi hata mfanya kazi wa ndani anahaki vilevile ambazo anahitaji kuzipata anapo kua akifanya kazi yake hiyo ili aweze kufaidika na kazi hiyo.

Tanzania na dunia nzima kwa ujumla inapiga vita dhidi ya ajira kwa watoto kwa maana yakuwa mtu akiwa chini ya umri wa miaka 18 haruhusiwi kuajiriwa bali anatakiwa apate haki yake ya msingi ya kupata elimu.

Mbali na dunia nzima kupinga suala hili katika nchi yetu ya Tanzania bado asilimia kubwa ya wafanya kazi wa ndani wako chini ya umri wa miaka 18 jambo ambalo ni kosa kisheria kwa kuwaajiri watoto hao.

Aidha wafanya kazi wa ndani ni watu ambao kwa asilimia kubwa huwa hawatendewi haki kwasababu huwa wanafanya  kazi kubwa huku wakilipwa ujira mdogo sana ukilinganisha na kazi wanazo zifanya.

Vilevile hakuna mikataba inayo walinda wafanyakazi hawa hivyo muajiri huwa anampangia vile anavyo jisikia na muajiriwa huyo hulazimika kufuata kile anacho pangiwa na muajiri wake.

Kipigo, matusi na udharirishaji huwakumba wadada hawa kutokana na umri  wao na hata wanapo jitetea bado waajiri wao wanakua siyo waelewa maana wao hutumia nguvu na mamlaka waliyo nayo katika nyumba yani baba au mama na wakati mwingine watoto wa nyumba hiyo.

Kilio na machozi yawa wafanya kazi wa ndani huishia kwenye geti la chuma na ukuta mrefu pamoja na nyumba yenye milango iliyo fungwa na madirisha yenye vioo vyeusi kama gari za kubebea watu maarufu pasipo kupata msaada wowote na muda mwingine huwekewa walinzi.

Pia asilimia kubwa ya wafanya kazi hawa hutolewa maeneo ya vijijini, watoto hawa huwaraghai kuwa wataishi maisha mazuri,maripo mazuri na hata huahidiwa kupelekwa shuleni jambo ambalo huwavutia waoto hao kufanya kazi hizo.

Nyuso za watoto hao hutabasamu pale wanapo fika mjini na kuona mataa kama waswahili wanavyo sema, jumba lenye geti,ukuta na madirisha ya vioo na ndani kukuwa na masofa  ya kisasa, Runinga ya kisasa,kipuliza upepo na vingine vizuri kama hivyo ambavya havipatikani maeneo ya vijijini.

Mabinti hawa nyuso zao hutanda giza na kukunjamana kama wazee wenye miaka 90 huku wakiwa na miaka kati ya 12-17 kutokana na kipigo pamoja na manyanyaso wanayo yapata ya kila siku wawapo katika majumba hayo ya kifahari.

Kutokana na umri wao wanashindwa kuchukua maamzi yaliyo sahahi kwao kama kutoa taarifa kwa majirani, viongozi wa serikali ama wazazi wao kutokana na vitishowanavyo pewa.na waajiri wao.

Wakati nikitokea Dar es salaam kueleke mkoa wa Kigoma kwa kutumia usafiri wa treni nilikutana na binti mwenye umri wa miaka 15 ambae hakupenda jina lake litajwe, Binti huyu ni mzaliwa wa Tabora wila ya urambo nilibahatika kukaa karibu nae na katika mangumzo yetu nilimuona kama binti mdogo lakini anasafiri akiwa peke yake nikaamua kufanya nae mahojiano.

Katika mahojiano  na binti huyo, binti alikua na haya ya kusema, “Nina miaka 15 ni mzaliwa wa Tabora wilata ya urambo na hivi unavoniona nimetokea mkoani Morogoro, nina miaka mitatu nikiwa nipo mkoani morogoro na nimekua nikifanya kazi za ndani. Kusema ukweli nimekua nikifanya kazi hii tangia nikiwa na miaka 13 lakini sijaona mafanikio yake kwa maana nimekua nikipokea manyanyaso makubwa, kipigo na matusi kutoka kwa waajiri wangu huku nikipewa ujira mdogo kiasi cha Tsh.15000 kwa mwezi na pesa hiyo nakuwa sipewi kwa wakati, niliyazoea maisha hayo japo nilikua siyapendi ndipo nilibahatika kutoroka nyumbani wiki mbili zilizo pita na kwenda kumueleza  mwenyekiti wa mtaa baada ya kuelekezwa ofisi yake ilipo  na baada ya kumueleza hayo alifika nyumbani ndipo nili mwenyekiti aka toa amri ya kulipwa ujira wangu wote pamoja na kupewa nauli ya kurudi nyumbani kwetu”mwisho wa kunukuu.

Aidha binti huyo nilipata kuongea nae mambo mengi sana na nikajifunza kuwa kuna watoto wengi wananyanyaswa sana kwa kivuri cha kufanya kazi za ndani katika jamii zetu.

Huyu ni mmoja kati ya mabinti wengi wanao kutana na mikasa kama hiyo na wengine hukutana na mikasa zaidi ya hii lakini  hushindwa kuzitoa sauti zao ili kupewa msaada zaidi ili kusaidiwa katika mikasa au manyanyaso kama hayo.

Mbali na manyanyaso hayo baadhi ya waajiri wao wa kiume wamekuwa wakiwahitaji kimapenzi na pengine hubakwa na waajiri wao na kuwapa vitisho vikali na mabinti hao huvumilia maana huogopa vitisho hivyo kutokana na umri wao mdogo.

Uelewa wa mabinti hawa kuwa mdogo na kukosa elimu hushindwa kutoa taarifa kwa majirani pamoja na mashirika yanayo jihusisha na kutetea haki za wanawake na watoto.

Mashirika mbalimbali yanayo tete haki za watoto wakishirikiana na jeshi la polisi wamekua wakitoa elimu juu ya mambo haya na wamekua wakitoa namba zao ili kuwapa taarifa za mambo kama haya lakini bado jamii haijaamka juu ya manyanyaso kama haya kwa watoto.

Mgawanyo wa mwenye nacho na asie kuwa nacho hii inawafanya baadhi yawatu kukjosa utuna kuwaona binadamu wenzao kama wanyama na kuwafanya unyama kama huo kwa watoto wasio na hatia.

Sitaki kuamini kuwa waajiri wote wanao waajiri wa wadada wakazi kuwa  wote wana roho za kinyama kiasi hicho bali na baadhi yao kwasababu kuna wengine ambao huwaajiri watu wazima na kuwalipa ujira wao vizuri na cha zaidi huushi kama ndugu.

Kilio cha binti wakazi wa kitanzani nipale anapo kosa haki zake za msingi na hasa kupewa ujira ambao haulingani na kazi anazopewa pamoja na kunyimwa uhuru wa kufanya yale anayo yapenda kuyafanya.

Jamii ielimike na kutambua kuwa kumuajiri mtoto ni kosa la kisheria na mfanya kazi wa ndani ana haki kama walivyo kua wafanya kazi wengine walivyo na haki wawapo kazini ikiwemo kupewa ujira unaolingana na kazi wanazo pewa.

Furaha ya binti wa kazi wa Tanzania ni ni pale tu atakapo wekewa mkataba wa kufanya kazi, haki zake za msingi pamoja na ujira wenye tija unao lingana na kazi anazo zifanya.

Mfanya kazi wa ndani anapaswa kuzijua haki zake za msingingi awapo kazini na pale anapo ona kuwa anakoasa haki zake za msingingi ni vyema akatoa taarifa katika vyombo husika ili aweze kusaidiwa haraka iwezekanavyo.

Na huu ndio mwisho wa makala yetu kwa leo ambapo tumekua tukizungumzia kilio cha binti wa kazi za ndani wa kitanzania ambapo tumeona changamoto anazo kutana nazo binti huyu wakazi na kubwa zaidi ikiwa ni kukosa haki zake za msingi.

Nikushukuru kwa kuchukua muda wako kusoma makala hii naamini umejifunza kitu na utakua barozi wa kutetea haki za watu hawa kwasababu naamini haya yapo mpaka mtaani kwako muokoe binti wa kazi za ndani kwa kutoa taarifa katika vyombo husika.

USIKOSE MAKALA IJAYO INAYO HUSU MIMBA ZA UTOTONI
Ø Maana
Ø Chanzo
Ø Madhara
Ø Suruhisho
Ø Maoni
KWA TUKIO AU TANGAZO LOLOTE TUTAFUTE KWA NAMBA. 0713 305 650





Chapisha Maoni

0 Maoni