NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Kulingana na
sheria za nchi yetu ya Tanzania ni kwamba mtoto ni Yule mwenye umri chini ya
miaka 18 yani kuanzia miaka 17 kushuka mpaka mwaka 0 hapa ndipo tunapata maana
ya neono mtoto.
Miezi
kadhaa iliyopita Rais mtukufu wa serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania
Dk. John Pombe Magufuli alitangaza kuwa katika serikali yake mwanafunzi atakae
pata ujauzito hato ruhusiwa kurudi shuleni tena na huku sheria ikisema kuwa
mwanaume atakae mpa njauzito mwanafunzi basi atafungwa miaka isiyo pungua 30.
Na
tunapo zungumzia neono mimba ni kiumbe ambacho bado kipo ndani ya tumbo ambacho
kinatarajiwa kuwa mtoto baada ya miezi tisa kutimia.
Basi
mpenzi msomaji wa makala hii nikukaribishe mojakwamoja katika makala hii ya leo
ambayo utapata kujifunza mengi na ambayo ulikua hujui na kama ulikuaunajua basi
tunakuongezea maarifa zaidi.
Tunapo
zungumzia mimba za utotoni ni zile mimba ambazo wanazipata watu ambao wako
chini ya miaka 18 na hii moja kwa moja zinakua ni mimba za utotoni.
Aidha
mimba za utotoni ni mimba ambazo zinapatikana kimakosa kwasababu haziruhusiwi
kisheria kwa mtu mwenye umri huo kuubeba ujauzito.
Sheria
ya nchi yetu ya Tanzania inapiga vita dhidi ya mimba za utotoni na huku bado
baadhi ya watu na hasa vijijini wamekua wakivunja sheria hii aidha kwa kujua
ama kwa kuto kujua juu ya suala hilo.
Kwa
mjibu wa sheria za nchi mwanamke anatakiwa ama anshauriwa kubeba ujauzito akiwa
a na umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea na hasa akiwa amesha olewa.
Nilibahatika
kufanya mahojiano na Aisha Athumani binti wa kizaramo aishie jijini Dar es
salaam ambae hakupenda kuchukuliwa picha yake wala mahali anapo ishi na wala
shule aliyokua akisoma alikua na haya ya kusema “Kwa majina naitwa Aisha Athumani naishi Dar es salaam nina miaka
16 nimeishia kidato cha kwanza baada ya kupewa ujauzito na mwanaume alie nipa
ujauzito aliamua kukimbia na mpaka leo hii hajulikani alipo istoshe kwasasa
siwezi tena maana nimesha kua mzazi na mtoto huyu unae muona ni mwanangu nalea
kwa sasa,baada ya kupata ujauzito huu nilifukuzwa shule na wazazi wakanifukuza nyumbani
wakasema nisipokuja na alie nipa ujauzito huo nisikanyage nyumbani kwao na hivi
unavyo niona naishi kwa neema ya Mungu na mwanangu huyu unae muona ndugu
mwandishi”
mwisho wa kunukuu.
Hatahivyo
Aisha hakuishia hapo aliongeza kwa kusema kuwa kilicho mponza na kupata
ujauzito huo kuwa ni tama zake mwenyewe kwasababu alilelewa katika malezi
mazuri, malezi ya dini hivyo anajutia kosa hilo linalo mfanya kuishi maisha
magumu kwa sasa.
Pia
aisha alitoa ushauri kwa watoto wa kike kuto kujihusisha na mahusiano ya
kingono kingali wadogo kwakua madhara yake ni makubwa na badala yake
wajihusishe na elimu na si vinginevyo.
Binti
Aisha ni moja kati ya mabinti wa kitanzania ambae amekutana na suala hilo lakini
tunapaswa kujifunza kupita yeye ili kuondokana na tatizo hilo la mimba za
utotoni.
Vilevile
kuna visababishi vya mimba hizi kupatikana na ni vingi sana lakini siku ya leo
tutapata kuzungumzia machache kati ya hauyo mengi yasababishayo mimba hizo za
utotoni.
Mila na tamaduni, sitaki kusema kuwa mila ndizo
husababisha mimba hizo hapa ukweli nikwamba mila nazo huchangia hili kwasababu
baadhi ya mila na tabaduni za kitanzania na hasa jamii za wafugaji huwa
zinaruhusu mabinti zao kuolewa wakiwa na umri mdogo nahii ikiwa ni ukosefu wa
elimu.
Tamaa, Ninapo zungumzia tama unzweza
usinielewe vizuri lakini maana yangu nikwamba unakuta binti kulingana na hali
ngumu ya kimaisha iliyopo nyumbani kwao anatamani kupata kitu fuani anajikuta
akijiingiza katika kufanya ngono akiwa na umri mdogo ili kupata kile anacho
kihitaji na hatamae anajikuta akipata ujauzito pasipo kutarajia.
Makundi rika,Binti anapokua katika hatua za
ukuaji huwa anapata marafiki wema na wabaya wa rika lake na anapo pata marafiki
wabaya basi anajikuta akishawishiwa na kujiiingiza kwenye mahusiano ya kingono
akiwa na umri mdogo na hatimae kupata ujauzizo.
Utandawazi, ujio wa sayansi na teknolojia katika karna hii ya 21
ime athiri sana maisha ya asili na kila mtu anaitumia teknolojia atakavyo
hususa ni matumizi ya simu kwa kiasi kikubwa simu zinatumika sana katika
mawasikiano hivyo ikitumika vibaya huwa mawasiliano hayo huwasababishia watoto
hao kupata ujauzito.
Uhuru kupita kiasi, binti anapo pewa uhuru wa kupita
kiasi basi binti hujisahau na kujiingiza katika mahusiano ya kingono nahii
hupelekea binti huyo kubeba ujauzito katika umri huo.
Basi
mpenzi msomaji wa makala hii hayo yalikua ni baadhi ya mengi yanayo sababisha
mimba za utotoni na umeweza kujionea ni
jinsi gani zinapatikana mimba hizo.
Vilevile
kuna madhara yatokanayo na mimba za utotoni hivyo leo hii tutaenda kuzungumzia machache kati ya
mengi ambayo huwapata watoto wa kike wanapo beba ujauzito katika umri huo.
Kuharibu ndoto, mtoto wakike anapo pata ujauzito
ndoto zake za maisha yake zinakua zimeishia hapo kwasababu anakua hana nguvu na
uwezo wa kufikiria maisha zaidi atafikiria kumlea mtoto wake.
Vifo, binti anapo pata ujauzito akiwa
chini ya umri wa miaka 18 viungo vyake vinakua havijakomaa hivyo muda mwingine
hupelekea mtoto huyo kujifungua kwa njia ya upasuaji napengine hupelekea kifo
cha mama na mtoto.
Maradhi, kumbuka kuwa binti huyu ni mdogo
na viungo vyake havija komaa na anapo jifungua mtoto via vya uzazi vinaweza
kuchanika na kusababisha maradhi kama fistula na mengineyo kama hayo.
Basi
msomaji wangu hayo ni baadhi ya mengi yanayo weza kumkumba mtoto wa kike pale
anapo beba ujauzito akiwa na umri mdogo maarufu kama mimba za utotoni.
Aidha
jamii inahitaji elimu ya kutosha juu ya mimba za utotoni ili kuokoa kizazi hiki
dhidi ya mimba za utotoni na kumuokoa mtoto wa kike wa Tanzania.
Vilevile
wazazi wanatakiwa kuwapatia malezi bora watoto wao kingali watoto ili wasiweze
kujiingiza katka vishawishi vya namna hii ambavyo ni vibaya kwa watoto wetu.
Pia
ningependa kuishauri jamii ya kitanzania kwa ujumla kutoa elimu kwa watu ambao
bado wana mila hizo potofu lengo ikiwa ni kutokomeza suala la mimba za utoni.
Tanzania
bira mimba za utotoni inawezekana tuungane kwa pamoja kupambana na suala hili
au mila potofu zilizo pitwa na wakati kwapamoja tukisimama twaweza.
Na
huu ndio mwisho wa makala yetu kwa leo nikushukuru kwa kuchukua muda wako
kusoma makala hii naamini kuna kitu umejifunza na kama ulikua unajua basi
umeongeza maarifa naamini utakua barozi wa kupinga suala hili la mimba za utotoni.
USIKOSE MAKALA IJAYO INAYO HUSU NDOA ZA
UTOTONI
Ø Maana
Ø Chanzo
Ø Madhara
Ø Suruhisho
Ø Ushauri
KWA TUKIO AU TANGAZO LOLOTE TUPIGIE KWA NAMBA 0713
305 650


0 Maoni