Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MVUA YAFANYA UHARIBIFU KATAVI

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Mvua zinazo endelea kiunyesha  katika kijiji cha isubangala na kata ya ilangu kwa ujumla wilaya ya katavi vijijini  imefanya uharibifu mkubwa wa mazao ikiwemo mahindi,maharage pamoja na tumbaku kutoka na mvua nyingi zinazo nyesha kila siku.

Aidha Bw.Living Sharutiel ni mkazi wa kijiji cha isubangala ameieleza plan media kuwa mvua hiyo imeleta madhara makubwa kiasi kwamba mazao yameharibiwa hususa ni maharage, mahindi pamoja na tumbaku.

Hata hivyo living ameieleza plan media kuwa kwa watu ambao waliweka mbolea kwenye mazao siku za hivi karibuni nisawa na kazi bure kutokana na mbolea hiyo kusombwa na maji.

Kwaupande wake Bi. Sifa Bartazal amesema kuwa mvua hizo zinazo endelea zinafanya shuguli nyingi kusimama huku wakishindwa kwenda shambani kutokana na mvua hizo kunyesha kila wakati.

Pia Bi. Brtazal ameongeza kwa kusema kuwa mito  imefurika maji jambo ambalo linawafanya washindwe kuvuka kuelekea sehemu mbalimbali kwasababu mito hiyo ina madaraja ya kienyeji ambayo walitumia miti kutengeneza hivyo kujaa kwa mito hiyo imesababisha madaraja hayo kusombwa na maji.

Bi. Bartazal amamaliza kwa kusema kuwa kwa wale wakulima wa tumbuku nyumba za kukaushia tumbaku [BANI] zinabomoka kila kukicha na ni hasara kubwa kwa wakulima hao kwasababu msimu wa kukausha tumbaku unakaribia.


Chapisha Maoni

0 Maoni