Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

TABU YA MAJI KIGOMA

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Wakazi wa eneo la uwanja wa ndege [airport] manspaa ya kigoma ujiji wamepaza sauti zao wakilalamikia tabu  ya maji inayo wakumba wakazi hao kwa muda mrefu mpaka leo hii.

Aidha Bi. Mwajuma Ally Mwinyi amesema mtaa huo umegubikwa na kero ya maji jambo ambalo huwalazimu kutumia maji ya visima wanavyo chimba ili kupata maji kwa matumizi ya majumbani.

Bi.Mwajuma ameongeza kwa kusema kuwa maji hayo si salama kwa matumizi ya majumbani hasa kwa matumizi ya kunywa kwani wanaweza kupata ugonjwa wa mripuko kama kichocho na kipindupindu.

Kwa upande wake Bw.Fred Hamenya kumesema kuwa waliahidiwa kuwa mapema mwezi huu mradi huu unge kamilika lakini mpaka leo hii hakuna dalili zozote za kupata maji safi na salama.

Pia Hamenya amemaliza kwa kusema kuwa kwa sasa wanaishukuru mvua inapo nyesha wanapata maji ya kunywa lakini katika kipindi cha kiangazi hulazimika kutumia maji ya kisima.


Vilevile wakazi hao wameiomba serikali kushughulikia tatizo hilo katika mwaka ujao wa 2018 ili kunusuru afya na maisha ya wakazi hao katika kulijenga taifa imara lisilo na maradhi. 

Chapisha Maoni

0 Maoni