Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MAJI BADO KITENDAWILI MOROGORO

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Wakazi waishio katika mtaa wa mazimbu rodi kata ya lukobe manispaa ya morogoro wameendelea kupaza sauti zao  wakilalamika juu ya tatizo la maji kuwa ni tatizo la muda mrefu mpaka sasa.

Aidha mmoja wa wakazi hao Bw. James Lyanga amesema kuwa maji katika mtaa huo yamekua kitendawili kisicho kua na jibu kwa muda mrefu sasa pasipo kufanyiwa utatuzi.

Vilevile Bw.Lyanga amesema maji huwa yanatoka mara moja tu kwa wiki napengine huwa hayatoki kabisa hata kwa muda wa wiki mbili jambo ambalo huwapa tabu wakazi hao.

Lyanga ameonesha kushangaa kuona maji yakiuzwa kwa kutumia magari[boza] pamoja na pikipiki za magurudumu matatu vibajaji]  “Ndugu mwandishi nashangaa kuona maji yakiuzwa kwa kutumia maboza pamoja na vibajaji huku nikishindwa kuelewa wao maji hayo wanayatoa wapi? Na kama wao wanayapata maana yake wahusika wameona kuwa wakiwauzia hao ndipo wanapata faida kuliko kutumia mabomba yaliyopo mtaani? Hayo ni maswali ambayo ndugu mwandishi wakazi tunakosa majibu” mwisho wa kunuku.

Lyanga amemaliza kwa kusema kuwa imekua tabia pale wananchi wanapo andamana huwa maji yanatoka na baada ya muda kidogo yanakua hayatoki tena.

Pia Bi.Edith Mushi amesema kutokana na shida hiyo ya maji wanalazimika kununua maji kutoka kwenye magari yanayo uza maji ambayo huuzwa kwa bei kubwa kati ya Tsh. 300- 500 kwa ndoo moja  kubwa.

Bi. Edith ameongeza kusema kutokana na hali ngumu iliyopo kwa sasa wanashindwa kununua maji mengi hivyo baadhi ya shughuli zinazo hitaji maji mengi kama kufua nguo kukwama.

Wakazi hao wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo kwasababu limekua kero na mateso kwa wakazi  hao na likiwa ni tatizo tokea muda mrefu.

Miezi mitatu iliyopita kituo cha plan media tulichapisha habari juu ya suala hili lakini  bado  kero hii haijafanyiwa ufumbuzi mpaka leo hii.








Chapisha Maoni

0 Maoni