Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

LAANA YA BABA, EPSODE-01


NA.GOODLUCK CHRISTOPHER,
Hii ni simulizi ya kweli iliyo tokea katika kijiji cha Katete Kata ya Mwakizega Mkoani Kigoma ambayo inamhusu Binti anae fahamika kwa jina la Anitha ambae alipata laana kutoka kwa baba yake mzazi tafadhali fuatilia kisa hiki.

 Nikukaribishe msomaji wangu katika simlizi hii fupi yenye kusisimua na mafundisha kwa jamii kutokana na mambo yanayo tokea katika familia zetu.

Kabla ya kuianza simulizi yetu tuanze na kumfahamu mhusika wetu. Anitha ni binti alie zaliwa katika kijiji cha Katete huko uvinza mkoani kigoma na ni mtoto wa kwanza katika familia yenye watoto sita huku watoto watatu wakiwa ni wakike na wakiume wakiwa ni watau pia kuanzia mtoto wakwanza mpaka wa tatu wote ni watoto wa kike kwa maana hiyo familia hii ilipata watoto wa kiume mwishoni kama mwenyezi Mungu alivyo panga.
 EPSODE-01
[WOSIA WA WAZAZI]…..Mwanetu tunakupeleka shule ili uje kuwa mwokozi wa familia yetu maana tumechoka na huu umaskini walisema wazazi wa Anitha wakati akiwa shule ya msingi Katete, Msijali wazazi wangu kwasababu ndoto yangu ni kuwa Daktari mkubwa tena wa kimataifa na nitakununulieni gari kila mmoja wazazi wangu lakini pia nitawajengea nyumba nzuri tena ghorofa yenye bwawa la kuogelea hapa nyumbani alisema Anitha. 

Tunafurahi sana mwanetu tunashukuru kwakua unafahamu umhimu wa kusoma na sisi tutafanya juu chini usome mpaka uitimize ndoto yako walisema wazazi wake.

Wazazi wa Anitha walikua ni wakulima wadogowadogo wanao tumia jembe la mkono hivyo waliongeza ukubwa wa mashamba lengo ikiwa ni kuhakikisha mtoto wao wanamtimizia ndoto yake na haki yake ya msingi ya kupata elimu na kumbuka kuwa wakati huo wadogo zake wawili walikua nao wamekwisha kuanza shule basi hata mahitaji yao yaliongezeka zaidi kutokana nakua wanafunzi walikua ni watatu hivyo wazazi walilazimika kununua sale,madafutari na ada ya Anitha pamoja na wadogo zake wawili ambao ni Vanesa na Agness.

Basi Anitha alihitimu masomo yake ya msingi na kufaulu vizurina kufanikiwa kujiunga na kidato cha kwanza  ambapo wazazizi wake walimpeleka kidato cha kwanza katika shule ya Luchugi Secondary School iliyopo huko uvinza mkoani Kigoma wazazi walifurahi sana kwa kuona mtototo wao kuendelea kupiga hatua hususa ni pale wakiikumbuka ahadi ya mtoto wao.

Basi Anitha aliendelea na masomo yake na alionekena mwanafunzi anae fanya vizuri darani lakini wakati huohuo wadogo zake walionekana kuto ipenda shule wakiwa bado wako shule ya msingi na kipindi Anitha amefika kitato cha pili mdogo wake Vanesa alihitimu elimu yake ya msingi na kufaulu lakini alikata kuendelea na elimu ya sekondari.

……..Nawaombeni msijisumbue kunipeleka kujiunga na kidato cha kwanza sijisikii kuendelea na kama mkinipeleka shule basi nitakula pesa zenu tu na sitokaa darasani hata siku moja alisema Vanesa akiwaambia wazazi wake, Sasa wewe unataka nini?  Walimuuliza wazazi wake, Nitalima tu wakati nikisubiria kuolewa, Basi wazazi walijitaidi kumshauri lakini binti alikataa kusoma dipo waliamua kumwacha achague alicho chagua.
Itaendelea……
N.B: Majina ya wahusika katika simulizi hii yemehifadhiwa kwasababu za kiusalama kwasababu hili ni tukio la kweli ambalo lilitokea miaka kadhaa iliyo pita hivyo nimeona si vyema kutumia majina harisi ya wahusika kwa hilo nitaomba radhi msomaji wangu.
KWA MAHITAJI YA NAKALA YA SIMULIZI HII WASILIANA NA KITENGO CHA MASOKO KUPITIA:
+255 713 305 650

KUPATA STORI,HABARI,ELIMU,BURUDANI NA DINI TEMBELEA MITANDAO YETU IFUATAYO:
BLOG.planmediatz.blogspot.com
Facebook.PMTV_TZ
YouTube.PMTV_TZ
Instagram.pmtv_tz
Twitter.channel_plan

PLANMEDIA©2018


Chapisha Maoni

0 Maoni