Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

LAANA YA BABA,EPSODE-02

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER,
TULIISHIA HAPA.
……… Nitalima tu wakati nikisubiria kuolewa, Basi wazazi walijitaidi kumshauri lakini binti alikataa kusoma dipo waliamua kumwacha achague alicho chagua.
#EPSODE-02
Siku zilienda na hatimae binti akapata mume akaolewa mvomero huko mkoani Morogoro na maisha yaliendelea akiwa huko na wazazi wakabariki ndoa hiyo lakini wakati huo Anitha alikua kidato cha tatu ambapo Agness nae alikua amekwisha maliza darasa la saba nae pia alikataa shule hivyo wazazi wake hawakuumiza kichwa walimwacha tu zaidi waliongeza nguvu kwa Anitha maana waliipenda ndoto yake.
Pindi Anitha anaendelea na masomo yake aliendelea kubadilika taratibu kitabia mara baada ya kuanza mapenzi ya kisirisiri na mwanafunzi mwenzie ambae alikua akiendelea kumlagai kwa kumpa vitu vidogo vidogo akajikuta amezama jambo ambalo lilimfanya ashuke kitaaluma akaanza kufanya vibaya darasani lakini familia haikupata kujua hayo kwani walimuamini mtoto wao kwa asilimia 100%  istoshe wazazi wake hawakusoma hivyo ilikua ni vigumu kukagua maendeleo ya mtoto wao.
Siku hazingandi  Anitha alihitimu kidato cha nne na kurudi nyumbani kusubiria matokeo yake na kumkuta mdogo wake akiwa nyumbani hivyo maisha yakaendelea huku wazazi wakisubiria kwa hamu matokeo yake ya kuendelea na kidato cha tano hatimae chuo kikuu.
Wakati akisubiria matokeo aliendelea kujihusisha na mahusiano ya kimapenzi na vijana wa kijijini hapo kwani alikua amesha kuwa na sugu lakini wazazi walipo pewa taarifa za binti yao hawakuamini zaidi waliona ni wivu wa watu wa kijijini hapo juu ya mtoto wao hivyo basi hii ilimlinda sana mtoto huyo.
Baadae kidogo matokeo yakatangazwa ikaonekana matokeo yake siyo mazuri ambapo alipata [FOUR YA 30] ambapo kwa kawaida ailionekana hana sifa za kuendelea na kidato cha tano wala chuo chochote cha ufundi isipo kuwa VETA, Lakini pia kijana ambae walikua na mahusiano nae shuleni alipata [FOUR YA28] Ambapo ilionekana kuwa anasifa za kujiunga na vyuo vya vya kati.
Basi kijana ilionekana kwao hakuna pesa ya kumsomesha ndipo aliunda mbinu ya kumlagai Anitha kwamba akawadanganye wazazi wake kuwa kuna chuo kimepatikana mkoani mwanza kinapokea wanafunzi mwenye FOUR YA 32 Katika taaluma ya afya yaani Nursing hivyo wazazi walijikusanya na kumpatia pesa kwaajiri  ya kumpeleka shule.
Itaendelea……
N.B: Majina ya wahusika katika simulizi hii yemehifadhiwa kwasababu za kiusalama kwasababu hili ni tukio la kweli ambalo lilitokea miaka kadhaa iliyo pita hivyo nimeona si vyema kutumia majina harisi ya wahusika kwa hilo nitaomba radhi msomaji wangu.
KWA MAHITAJI YA NAKALA YA SIMULIZI HII WASILIANA NA KITENGO CHA MASOKO KUPITIA:
+255 713 305 650

KUPATA STORI,HABARI,ELIMU,BURUDANI NA DINI TEMBELEA MITANDAO YETU IFUATAYO:
BLOG.planmediatz.blogspot.com
Facebook.PMTV_TZ
YouTube.PMTV_TZ
Instagram.pmtv_tz
Twitter.channel_plan

PLANMEDIA©2018


Chapisha Maoni

0 Maoni