Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

KUMBILAMOTO,’’ KAMPENI ZA WAPINZANI SARAKASI ZA USIKU’’


NA.RASHID HASSAN
 Kumbilamoto aziita kampeni za wapinzani sarakasi za usiku.  MGOMBEA ngazi ya Diwani kupitia Chama cha Mapinduzi CCM ,Omary Said Kumbilamoto, amesema kwamba kampeni zinazofanywa na wapinzani wake ni sawa na sarakasi za usiku ambazo hazionekani mpaka ziwashiwe taa.

 Amesema kwamba wapinzani hao wamekuwa wakitumia mgongo wake katika kuomba kura kwa wana nchi jambo ambalo  amelifananisha na sarakasi za usiku ambapo zikiwashwa taa ndio zinaonekana "" Hawa jamaa zangu ni watu wa ajabu sana, kwa sasa hawana jipya kwani kilichobakia ni siasa za sarakasi, Mimi ni taa hivyo hawawezi kuonekana mpaka niwake hivyo sitojali na watazidi kupata tabu sana na Mimi"amesema Kumbilamoto.

  [pichani ni Ndugu Omary Said Kumbilamoto akitoa sera zake mbele ya wananchi waliohudhuria kwenye viwanja vya shule ya KOMBOvilivyopo vingunguti}.

Aidha, amewaomba wakazi wa Vingunguti wasitishike na vitisho vyao kwani wanatapatapa hawana njia ya kujificha. Pia amewaomba wazidi  kumjengea imani ili wamchague tena kwa ajili ya kuwatumikia wana nchi hao kwani chama alichokuwa nacho kwa sasa kinatekeleza ilani na Sera zake zinaeleweka.

Naye Mbunge wa Jimbo la  Segerea , Bonnah Kaluwa, amewaomba wana nchi wamchague Kumbilamoto ili hata yale mambo yaliyokuwa yakishindikana kupitia Baraza LA madiwani yaweze kupita kwa urahisi. " Jimbo langu  hakuna hata mwakilishi kutoka chama cha CCM, hivyo mkiniletea Kumbilamoto mtanirahisishia kazi.


   [Pichani ni Mbunge wa Jimbo la Segerea,Mh Bonna Kaluwa akinadi sera za mgombea udiwani kupitia chama cha Ccm ,Picha na Rashid Hassan.]

 Mbali na hayo, amesema mpaka sasa Serikali imetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya kufanya upanuzi wa zahanati ya Mnyamani kuwa kituo cha afya.
 Katika hatua nyingine, aliyekuwa mwanachama  wa Chadema  ambaye alikuwa katika ngazi mbali mbali ikiwamo mkuu wa Idara ya ulinzi na usalama  mkoa wa Dar es Salaam.

Pamoja na mwenyekiti wa Jimbo La uchaguzi Ukonga, Kidera Gango, amesema kauli za wapinzani za kusema wamenunuliwa zipuuzwe kwamba wao walijiondoa kuunga juhudi za Mh Rais Magufuli" Kweli tumenunuliwa lakini sio kwa fedha, kununuliwa kwetu kumetokana na Sera nzuri za CCM pamoja na ilani yake inayotekelezeka"amesema Gango

 Pia amesema kwamba, ccm ni chama pekee chenye ilani na kwamba vyama vingine viliungana na kujitengenezea karatasi zenye malalamiko huku wakiziita ni Sera zao





Chapisha Maoni

0 Maoni