NA,RASHID HASSAN

Pia amesema Omary ni mchapakazi na wao kama
chama hawakufanya makosa kumpisha Kumbilamoto kwani wanajua kero zitataturika
kwa haraka tofauti na alivyokuwa upinzani . " Niwaambie kitu, Sera za
wapinzani ni kutofanya kazi na serikali , sasa kama huwashirikishi hao
maendeleo yatakujaje? Sasa msifanye makosa tuleteeni Kumbilamoto Vingunguti mfaidi
matunda

Katika
hatua nyingine , Mbunge wa Ilala Mh Zungu, amesema kuwa ccm hawanunui kura wala
watu Bali wanashinda kwa ajili ya kuwajali watu.
Amesema kuwa wao kama chama hawachagui watu
kwa ajili ya kuuza sura , wanachokiangalia ni uwajibikaji na kujali kero za
wananchi. Pia amewataka wakazi hao kumchagua Kumbilamoto kwani tayari
ameshawasiliana na viongozi wa Serikali TAMISEMI pamoja na Waziri wa Maji na
Ujenzi watakwenda Vingunguti wiki ijayo ili kutatua kero katika sekta hizo alizo
zitaja. Hata hivyo , Julius Mtatiro, amesema kuwa chama cha CUF kimeguka
vipande vipande hivyo aliona ni vyema akatafuta jukwaa sahihi la kutatua kero
za wananchi na maskini ambapo ni CCM.
Amesema kabla ya Kumbilamoto kujinga na ccm, alikuwa kiongozi pekee wa udiwani mchapakazi kuliko Madiwani wote wa upinzani. " Ndugu zangu nimekaa CUF miaka 10, miaka yote niliyokuwepo sijaona mafanikio zaidi ya migogoro, Sasa nikiongeza miaka 10 mingine nitapoteza uelekeo wangu wa Kisiasa njia sahihi nikajiunga na CCM kwa matakwa yangu binafsi na wala sijanunuliwa kama Maneno yanavyozidi kusemwa "amesema Mtatiro.

Naye Mbunge wa Segerea Bonnah Kaluwa, amewaomba wakazi wa Vingunguti wampatie Kumbilamoto kwani katika Jumbo lake hakuna mtu wa ccm hivyo ni vigumu kupitisha bajeti za maendeleo mbele ya wapinzani. Katika hayo, Mgombea Udiwani Kumbilamoto , ameomba kura zake huku akizidi kuwaahidi wananchi wake maisha bora watakapo mchagua tena


Shamra shamra za Kampeni zikizidi
kunoga na kuelekea tamati , leo tumeshuhudia baadhi ya Vigogo wakubwa
wenye nyadhifa CCM , wakijitokeza kwa wingi kumnadi Mgombea ngazi ya Udiwani
aliyekuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Kata ya Vingunguti Omary
Kumbilamoto katika Kampeni za kutetea kiti chake kupitia CCM.
Miongoni Mwa Vigogo waliohudhuria ni pamoja na
Mwenyekiti wa Wazazi Taifa , Dr Edmund Bernard Mndolwa, Katibu wa Wazazi Taifa
Ndugu Erasto Sima, Sangara Mjumbe Kamati ya Utekelezaji Wazazi Mkoa wa Dar es
Salaam, Mbunge wa Segerea Mh: Bonnah Kaluwa , Mbunge wa Ilala , Mh Zungu,
Julius Mtatiro aliyetoka CUF pamoja na Viongozi wa ngazi mbalimbali.
Katika kuona Ccm inapata ushindi, Mgeni rasmi
Edmund Bernard Mndolwa, amesema huu ndio wakati wao wa kumchagua Kumbilamoto
kuwa Diwani wao ili akashirikiane vema na Serikali katika kutatua Kero za
Wananchi.

Amesema kabla ya Kumbilamoto kujinga na ccm, alikuwa kiongozi pekee wa udiwani mchapakazi kuliko Madiwani wote wa upinzani. " Ndugu zangu nimekaa CUF miaka 10, miaka yote niliyokuwepo sijaona mafanikio zaidi ya migogoro, Sasa nikiongeza miaka 10 mingine nitapoteza uelekeo wangu wa Kisiasa njia sahihi nikajiunga na CCM kwa matakwa yangu binafsi na wala sijanunuliwa kama Maneno yanavyozidi kusemwa "amesema Mtatiro.

Naye Mbunge wa Segerea Bonnah Kaluwa, amewaomba wakazi wa Vingunguti wampatie Kumbilamoto kwani katika Jumbo lake hakuna mtu wa ccm hivyo ni vigumu kupitisha bajeti za maendeleo mbele ya wapinzani. Katika hayo, Mgombea Udiwani Kumbilamoto , ameomba kura zake huku akizidi kuwaahidi wananchi wake maisha bora watakapo mchagua tena


0 Maoni