Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

SAFARI YA BISHOP JOSHUA KATIKA MUZIKI



SAFARI YA BISHOP JOSHUA KATIKA MUZIKI
Hii ni historia fupi ya muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania anakuja kwa kasi ndugu Yoshua Mbonabucha maalufu kama Bishop Joshua ni muimbaji ambae amejaaliwa kipaji na sauti yenye mvuto na uwezo wa kutunga nyimbo zenye ujumbe mzuri na uoako katika kuihubili injili kamili ya Mungu.
Muimbaji huyu alianza rasimi uimbaji wake mnamo mwaka 2014 ambapo alikua akiimba muziki wa kidunia au mziki wa starehe za dunia yaani muziki wa kizazi kipya [Bongo fravour] alifanya muziki huo kwa muda wa mwaka mmoja na kujizolea umaalufu katika muziki huo japo lilikua siyo kusudio la Mungu kuimba muziki huo.
Mnamo mwaka 2015 aliamua kuacha muziki wa kidunia ndipo aliokoka na kujiunga kwenye kwaya ya kanisa la E.A.G.T MPIJI MAGOHE mkoani Dar es salaam akaendelea kumtumikia Mungu kwa njia ya umbaji alipokelewa vizuri na uongozi wa kanisa wakamlea kiroho ndipo alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwaya katika kanisa hilo.
Mnamo mwaka 2016 aliamua kuimba kama muimbaji binafisi ndipo aliamua kuanza kurekodi nyimbo tano ambazo kiukweli ni nyimbo ambazo ukizisikiliza zina ujumbe kamili kuanzia majina ya nyimbo hizo ujumbe na hata sauti yake ya uimbaji wake miongoni mwa nyimbo hizi ni hizi zifuatazo hapa chini;
1:MKONO WA BWANA
2:IMANI
3:AMINI
4:DAKIKA 90 na
5:KWA NEEMA
Mwaka huu amebahatika kukamilisha albam kwa kurekodi wimbo mmoja ambao unafanya vizuri katika ulimwengu wa injili kwa hivi sasa unaofahamika kwa jina la MWAGA BARAKA na wimbo huu ndio umebeba jina la albam na albam hii ipo katika mfumo wa  audio.
Ukizihitaji nyimbo hizi znaatikana katika mfumo wa Adio CD na mitandao ya kijamii kama google account yake ya mbonabuchajoshua@gmail.com au WhatsApp namba yake ya 0714598392 ukifanya mawasilianohayo unajipatia nyimbo zote hizo naamili utabarikiwa nazo.
Muimbaji huyu yuko tayari kwa miaaliko mbalili mbali ya kanisani matamasha n.k hivyo kama unahitaji aje kuhudumu mahali ulipo yupo tayari kufika ili kuihubiri injili kamili ya Mungu chakufanya ni kuwasiliana nae kwa namba 0714598392.
Bishop Joshua ameshawahi kuhudumu katika matamasha tisa na mikutano ishirini na moja  badhi ya matamasha aliyo hudumu ni uzinduzi wa Maria Matha Charles albamu ya Kwaanini Mimi,Uzinduzi wa albamu ya Deborah Kihanga ya Nimemuona Bwana n.k
Bishop Joshua anamshukuru Mungu ndugu jamaa na marafiki kwa kumwezesha kufika katika hatua aliyoifikia vilele anaomba kwa taasi,kampuni au mtu mwenye uwezo wa kumsaidia kufanya video ya albam hii kwakua yeye hanauwezo wa kulipa gharama hiyo kwa sasa ukilinganisha yeye bado ni mwanafunzi wa kidato cha sita hivyo ukiguswa na huduma hii mtafute ili kuifikisha injili mahali inapotakiwa kufika kupitia huduma aliyonayo kijana huyu.

Chapisha Maoni

0 Maoni