Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

KIMBUNGA CHAUA WATU SABA





KIMBUNGA CHAUA WATU SABA
 

Kimbunga chasababisha uharibufu mkubwa katika eneo la Caribbean  ambapo mali nyingi zimeharibiwa na kimbunga hicho ikiwemo kupelekea watu saba kupoteza maisha , kimbunga hicho kinacho fahamika kwa jina la Irma kilikumba kisiwa hicho na kusababisha watu washindwe kuishi huku maafisa wakionya kuwa maeneo ya kisiwa cha ST.Martin kinacho milikiwa na uingereza kimeharibiwa kabisa.

 

Jitihada za uokoaji zinagonga mwamba kutokana na ugumu wa kupata maeneo mengine, wakati huo huo upepo umekua na nguvu na kuzalisha vimbunga viwili, kimbunga hicho cha kiwango cha tano kinatajwa kuwa ni kiwango cha juu na sasa kinapita kaskazini mwa Puerto Rico.





Nusu ya wakazi wa Puerto Rico hawana umeme baada ya kimbunga hicho kusababisha mvua kubwa inayo ambatana na upepo mkali  huku maafisa wakisema huenda umeme ukawa tatizo kwa siku kadhaa, Kimbunga hicho kilikua na kasi ya kilomita 295 kwa saa ambapo kilikadiliwa kupita katika pwani ya Dominica .

Chapisha Maoni

0 Maoni