Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

WATU WANNE WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUTAKA KUJIUNGA NA AL-SHABAB



WATU WANNE WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUTAKA KUJIUNGA NA AL-SHABAB
 
 Jeshi la polisi nchini Kenya linawashikilia raia wanne kutoka nchini Burundi wanaodhaniwa kuwa walikua wanaelekea nchini Somalia kujiunga na kundi la kigaidi la Al-Shabab, Maafisa wa ujasusi walikuwa wakiwafuatilia raia hao baada ya kupata taarifa kuhusu mipango yao, kwa mjibu wa msemaji wa polisi George Kinoti.
Ameongeza kwa kusema washukiwa hao wanne walikamatwa katika kizuizi cha polisi mjini Isiolo kilometa 350 kasikazini mwa mji wa Nairobi wakielekea mpakani mwa mji wa Mandera.
Pia maafisa wa ubarozi wa Burundi mjini Nairobi wanasema watatoa taarifa kamili kuhusu kukamatwa kwa raia hao wanne baada ya kushauriana na mamlaka husika katika nchi ya Kenya
Tukio kama hili si lakwanza kutokea nchini Kenya,  mnamo mwezi  Janury mwaka 2017 raia wa kigeni kutoka nchi ya Tanzania alikamatwa katika mji wa Mandera alipokua akijaribu kuvuka mpaka kuelekea Somalia kwa lengo la kujiunga na kundi lakigaidi la Al-Shabab.

Chapisha Maoni

0 Maoni