Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

SURUHISHO LA AJIRA KWA VIJANA TANZANIA



SURUHISHO LA AJIRA KWA VIJANA TANZANIA
 
 Karibu katika makala fupi ya leo ambayo nimekuandalia naamini unaenda kujifunza kitu kipya kupitia makala hii na kama unajua basi nakuongezea maarifa zaidi,  mada ambayo tunayo izungumza katika siku ya leo ni ajira kwa vijana wa kitanzania na hata wasio watanzania pia inawahusu kwasababu suala la ajira halitofautiani sana katika nchi zetu hususa ni za ki afrika. Karibu katika somo la leo na kama utakua na maoni au ushauri utatuandikia hapo chini mwishoni mwa makala hii.
Ajira nini?
Ajira ni shughuli harari anayo ifanya binadamu kwa ajili ya kumuingizia kipato au malipo yanayo lingana na shughuli husika anayoifanya binadamu huyo, hii ni maana moja ya neon ajira japo kuna maana nyingi za neon hilo ila kulingana na muda naomba tutumie maana hii na kama una maana nyingine ya neon hilo siyo dhambi ukiitumia ilimladi tusipoteze maana.
Kuna aina mbili za ajira ambazo ni kujiajiri na kuajiriwa nisikupotezee muda kwa kuelezea kiundani maana ya hizi aina za ajira huu ulikua ni utangulizi wa kukuweka karibu ili kukuweka karibu kwa kile ambacho naenda kukizungumza siku hii yaleo.
Niombe radhi  kwa waajiri wote popote mlipo kwakua leo nataka nitete na vijana wenzangu kuwa na mawazo ama kujikita zaidi katika suala la kujiajiri kuliko kutegemea saana kuajiriwa naamini vijana mko na mimi katika hili lakini simanishi ndo muache kuajiriwa hapana soma kwa makini na taratibu utanielewa nini namaanisha.
Tatizo la ajira limekua tatizo kwa sisi vijana hasa vijana wakitanzania na hiki ndicho kimenipelekea kuandaa makala hii ili vijana wenzangu muweze kuamka na kutambua ni jinsi gani ya kupambana na hali hii ya tatizo la ajira kwetu sisi vijana.
 

 Tatizo la ajira halipo Tanzania tu bali lipo mataifa mengi tu na hata mataifa yale mnayo yasifu kuwa yameendelea sitaki nielezee sana kati mataifa mengine kwakua leo tunazungumzia taifa letu hivyo kama ulikua hujiui  chanzo kikubwa cha tatizo la ajira Tanzania basi jua kuwa ni mfumo wa elimu tuliokuwa nao.
Niombe radhi kwa Mh. Ndalichako maana hii ni wizara nyeti ila naomba tu kwa leo nijaribu kuwaelewesha watanzania, ni ukweli usiopingika kuwa mfumo waelimu tulionao ni chanzo kikubwa cha tatizo la ajira Tanzania najua kuna wasomi wakubwa sana mna PHD mnaanza kubisha kwa ninachokiongea leo maana mwenzenu sikupata nafasi ya kusoma saana japo nina elimu ya asili .
Nikushukuru  baba mwenye nyumba kwa kutuletea elimu bure bila kusahau kauri mbiu yako nzuri unayoitumia ya hapa kazi tu! Naile ya “serikali ya viwanda” Kwa mjibu wa kitabu cha Mungu niinachokitumia kinasema “asiefanya kazi na asile” kwa maana hiyo asie fanya kazi akila anakua ametenda dhambi.
 

 Elimu bure wazazi mmejitahidi kupeleka watoto shule nikijaribu kutembelea shule kadhaa nakuta shule zimejaa wanafunzi kuanzia darasa lakwanza mpaka kidato cha nne ila naasikia wasome wakijua serikalini hakuna ajira siwatishi wazazi ambao mna watoto wanao soma leo nimeamua niwaletee dawa ya tatizo la ajira kwa vijana wa kitanzania basi usichoke soma mpaka mwisho upate dozi kamili.
Katika mfumo wa elimu tunao utumia kwa sasa ni kuanzia Chekechea[Nursary],msingi[Primary],Sekondari[Secondari] pamoja na Vyuo[Coledge & Univercity] huu ndio mfumo ambao huwa unatumika katika kuwatengeneza vijana kuwa wasomi ikizingatiwa kwa sasa elimu ya msingi na sekondari ni bure hivyo tunapata vijana wengi wasomi wasio na ajira hapo baadae kama hatutofunguka macho mapema.
 
 Katika mfumo huu wa elimu haumjengi kijana katika kujiajiri bali mfumo huu unamjenga kijana katika mazingira ya kuajiriwa walimu wenzangu mtakua mashahidi wa hilli  maana sisi ndio hushinda na vijana hawa na hatimae tunakua tunazalisha vijana ambao hawna mawazo ya kujiajiri kulingana na mitaala na mfumo huu unao tuimika kwasasa.
 

 Lazima tutambue kuwa zama zinabadilika miaka ya nyumba sana kulikua na mazoea kwamba mtu anapokua amesoma basi ajira zinakua njenje kwakua kulikua na uhitaji mkubwa wa wafanya kazi, katika zama hizi nikwamba idadi ya wasomi imeongezeka ofisi ni zilezile hivyo inakua ngumu kila mtu kupata nafasi ya kazi kama iliovyokuwa zamani vilevile idadikubwa ya wasomi inapelekea wasomi wengi kukosa nafasi za kazi na kubakia mtaani.
Lazima tukubari kuwa tunaudhaifu wa sekta husika ikiwemo na sisi raia wenyewe bila kusahau wazazi mnao wasomesha watoto wenu kuwa hakuna mfumo elekezi wa kuwajenga watoto ama wanafunzi katika kuwajengea mawazo na ujuzi wa kuweza kujiajiri mala baada ya kuhitimu elimu yao hivyo ni muda sasa wa kubadilika na kutambua udhaifu huo.
Juzi wakati nikiwa kwenye daladala nilikutana na kijana mmoja mwenye umri wa miaka 25 akiwa ameshikiria bahasha ya kaki alikua amevaa nguo safi na kiatu kizuri sana lakini kwa mbaali alionekana  kama amechoka hivi  kwa bahati nzuri nilikaa siti ya karibu yake nilimsalimia akaniitikiasalammu yangu ndipo nikapata nafsi ya kuzungumza nae nikamuuliza kaka unafanya kazi ofisi gani? Akajibu”sina kazi” nikamuuliza umetoka wapi? Akajibu “nimetoka ofisi Fulani (sipendi niitaje kwasababu za kiusalama) akaendelea kusema nilikua nimepeleka barua ya kuomba kazi lakini imeshindikana na ni mwaka watatu natafuta kazi chaajabu sijapata, nimemaliza chuo mwaka juzi na haya mavazi unayoona nimevaa nimeazima kwa rafiki yangu yani hii nchi we acha tu” tuliendelea kuongea nae mambo mengi kaka yangu yule hatimae nikafika kituo kilichofatia nikashuka yeye akaendelea na safari yake huu ni mfano tu ila naamini tuna vijana wengi sana wa aina hii naamini mmeanza kunielewa sasa.
 

 Naongeqa na wewe kijana mwenzangu, kaka yangu, mdogo wangu na hata nyie wazazi wetu mnao tusomesha juu ya tatizo la ajira kwa vijana, hebu tujifunze kwa mataifa mengine yaliyo endelea kwamba wao walifanikiwa vipi katika hili utakuta kwamba wao wametengeneza mifumo mizuri ya kuwajenga vijana wao katika mazingira ya kujiajiri kuanzia ngazi ya familia na hasa kati umri mdogo.
Nikisema kuwajenga vijana katika mazingira ya kujiajiri wengine hawanielewi na wengine wateleta sababu kwamba wazazi wenyewe wana miaka kedekede wakiwa katika kazi za kuajiriwa na watawezaje kuwajengea mazingira ya kujiajiri watoto wao na hali kuwa kipato chao ni duni? Hili ni swali ama hoja ambayo haina msingi wowote, kwa imani yangu ni kwamba inawezekana kama unafatilia makala hii kwa makini.
Lakini pia mfumo wa elimu katika nchi yetu unaangalia mtu amefauru nini? na siyo mtu anajua nini? hivyo mtu anapo fauru mtihani haijalishi amekariri huhesabiwa mojakwamoja anafaa hivyo mtu anapo fanya vibaya katika mtihani haijalishi anaweza na anajua nini? mojakwa moja huonekana hana kitu kichwani jambo ambalo siliamini sana na ndo chanzo kikibwa cha watu kukosa ujuzi wakufanya mambo mengine hasa kujiajiri jambo ambalo ni tofauti na mataifa yaliyo endelea.
Katika uumbaji Mungu alimuumba kila mwanadamu kwa jinsi ya pekee na kipaji ama uwezo wapekee wakufanya jambo fulana na kwa bahati mbaya hatuna utamaduni wa kuthamini vipaji vya watoto wetu wakati hivi ndivyo vingeongeza uwezo wa vijana wetu kujiajiri kwakua mtu anakua anafanya kitu ambacho anakiweza na anakipenda yani kwa uwezo aliojaliwa na mwenyezi Mungu.
Nisielezee sana suala vipaji maana siyo somo la leo ila nilikua nataka nikuvute karibu uweze kunielewa kwa undani kipi nazungumza japo kipaji ni sehemu ya mtu kujiajiri, kuna furusa nyingi sana ambazo zinatuzuynguka vijana katika nchi yetu ya Tanzania kwamfano kilimo na ujasilia mali kwa ujumla lakini pia kuna furusa nyingi tu hapo ulipo sema hujadhamilia kuzifanyia kazi.
Kilimo ni sekta pana sana ambayo inaweza kubeba ajira maelufu kwa vijana tatizo kubwa nikwamba vijana wengi na hasa wasomi hawana mawazo ya kugundua kama kilimo kinalipa sana, enzi za mwalimu J.K. Nyerere alianzisha kauli mbiu ya kilimo ni uti wa mgongo ambayo kwasasa imebaki kuwa ni hadithi, nahii sababu kubwa ni mchango wa serikali katika hili kwasababu wakati mkulima analima serikali  haipo akivuna tu serikali inaanza kuonekana hivyo hupelekea vijana kuona kilimo hakina manufaa kwao hatimae siku hizi wazee na kina mama ndio utawakuta kwenye masuala ya kilimo.
 Vilevile vifaa vinavyo tumika ni duni ambavyo sanasana ni majembe ya mkono na kupelekea vijana wengi kuchukizwa na kufanya kazi za kutumia nguvu sana lakini pia vifaa na pembejeo bado ni tatizo kubwa, nisielezee sana kuhusu kilimo maana lengo letu ni kupata suruhu ya tatizo la ajira kwetu vijana.

Ifike muda tuzione changamoto tulizo nazo na kuweza kupambabna nazo na siraha peke ya kupanda na hali hii ni mawazo chanya kwetu sisi vijana na hasa ikizingatiwa walio wengi mnajiita wasomi kutokana na vyeti mlivyo vipata vyuoni , nijambo la kushukuru kwakua tumeishia darasa lasaba, basi tumalizie kwa kuangalia vitu gani tufanye ili tujiajiri.
MAMBO YA KUFANYA ILI KIJANA KUJIAJIRI
Haya ni baadhi ya mambo ambayo kijana akiyafanya anaweza kujiajiri kwa kutumia mtaji aliokuwa nao maana mtaji wakwanza ni afya njema na akili au mawazo ulivyo jaliwa na Mungu tangia pale ulipo zaliwa na asmini kuwa mtaji ulio nao hakuna tajiri mwingine duniani mwenye nao karibu sana soma kwea makini uelewe usipo elewa unaruhusiwa kuuliza name nitakujibu haraka iwezekanavyo.
1:Weka cheti pembeni
Simaanishi ukitupe cheti chako lahasha maana kitahitajika mala baada ya kukamilisha malengo yako ya kujiajiri, maana yangu kubwa nikwamba ukitaka kujiajiri usiangale thamani ya cheti ulichonacho kwasababu utashindwa kuchukua uamzi huo wa kujiajiri maana cheti chako kitakutaka upate kazi kwenye kiti cha kuzunguka kuingia kazini saa 2 asubuhi na kutoka saa 9 mchana.
2:Angalia furusa ama kile unacho kipenda
Inabidi uangalie furusa iliyopo katika mazingira uliyonayo kuzunguka au lazima uangalie kilichopo ndeni yako au kipaji ama kile unacho kipenda, kwani kile alichokuwekea Mungu ndani yako alikua na kusudi la wewe kufanikwa hivyo ukifanya kinyume utajishangaa unazeeka ukiwa hujafanikiwa hata kidogo na hiki ndicho wengi hawakifahamu na wengi wao wanakaa na kupiga kelele kwamba maisha magumu na hali kuwa utajiri undani yao.
3:Chagua furusa
Lazima uchague furusa moja wapo amayo unaona kwamba itakufaa katika kuzishi ndoto zako maana utakapo kosea kuchagua itakusababishia kutozifikia ndoto zako maana utakua unafanya kitu ambacho unajilazimisha na hueendani nacho hivyo ni vizuri ukawa makini katika kuchagua hiyo furusa ili uweze kuziishi ndoto zako.
4:Fanya uchunguzi
Baada ya kuchagua hiyo furusa inabidi uifanyie uchunguzi kwa wengine ambao wanaifanya na kama karibu yako haipo kubali kuingia gharama za kwenda waliko kufanya uchunguzi huo na ikishindikana kabisa jaribu kutumia mitandao maana siku hizi tumerahisishiwa mambo itakusaidia kupata jawabu kwa haraka na vyepesi  kusonga mbele katika kuifanyia kazi furusa yako.

5:Fanya tathimini
Baada yakuona kuwa furusa hiyo inakufaa fanya tathimini kwamba je,furusa hiyo itakulipa au utaonekana tu kuwa umejiajiri pasipo kufaidika na furusa yako? hili ni jambo la msingi maana tunajiajiri ili tufaidike na tunacho kifanya na ndo maana kubwa ya kujiajiri, hivyo inakupasa kuwa makini katika hili kwa manufaa yako.
6:Chukua maamzi
Baada ya kugundua kama furusa inakulipa unapaswa kuchukua maamzi magumu ya kufanya kazi kwa kuthamiria maana kwa kila jambo ni lazima kuchuka maamzi ili kulifanikisha maana hakuna kazi inayo fanyika pasipo kuiamru akili yako kufanya maamzi.
7:Tenga muda maalumu
Baada ya kuamua unapaswa kutenga muda wa kufanya kazi zako usikubali kupoteza muda wako bure na kama ukishindwa kuzingatia muda utashangaa mambo hayaendi kwakua utakua umeshindwa kuzingatia na kuheshimu muda wako, wahenga walisema muda ni mali hivyo muda nao ni sehemu ya kukufanya ufanikiwe katika kazi zako.
8:Thubutu
Baada ya kuheshimu muda sasa ni kazi inaanza maana mpaka hapo umesha elewa kwamba unafanya kazi ambayo unaamini itakufikisha pale unapohitaji kufika na ikizingatiwa kwamba unafanya kitu ambacho unakipenda kwa moyo wako wote na Mungu atili baraka zake katika kazi yako.
9:Bidii
Baada ya kuifanya hiyo kazi usiishie kuifanya tu bali lazima ujibidishe maana  bidii huleta uvumilivu na mafanikio maana vijana wengi wanapenda kazi za kulalka masikini na kuamka tajiri ila nakuhakikishia kwamba hakuna kazi harari ya hivyo isipokua kazi haramu ambazo zinamchukiza Mungu na watu ambazo huwapeekea wengi kupotezamaisha mapema mno.
10:Kuwa na kisi
Hii ni sehemu yenye utata kidogo maana vijana wengi hatuna kiasi cha kufanya mambo yetu kwamfano watu wengi wanashindwa kufanikiwa kwasababu ya anasa na ninapo zungumzia anasa hili ni suala pana ambalo nisinge penda kulizungumza kiundani kwa leo, ninapo zungumza uwe na kiasi namaanisha matumizi yako ya Chakula,Malazi na Mavazi visizidi uwezo wa kipato chako maana utashindwa kuiendeleza kazi yako, hivyo unapaswa uwe na kiasi katika hayo.

Na huu ndio mwisho wa makala yetu kwa leo naamini kuna mambo umejifunza na kuongeza maarifa ila usikose katika somo litakalo fuatia chakufanya ni kuendelea kutembelea mitandao yetu ili usipitwe na somo lijalo vilevile kama unahitaji nakala ya somo hili inapatikana chamsingi ni kuwasiliana nasisi tuone jinsi gani ikufikie namba ya kuwasilana nasisi ni 0713305650.

Kwa maoni au ushauri tuandikie hapo chini au tuandikie kupitia email yetu planmediatz@gmail.com ama namba yetu ya simu 0713305650 itakua vizuri sana hii ni Plan Media way to success.


TANGAZA NA PLAN MEDIA KWA BEI NAFUU SANA
TEL: +255 713 305 650
 
 WOTE MNAKARIBISWA     

Chapisha Maoni

0 Maoni