Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

WAKIMBIZI WAISHIO TANZANIA WAANZA KUREJEA NCHINI BURUNDI



WAKIMBIZI WAISHIO TANZANIA WAANZA KUREJEA NCHINI BURUNDI


  Wakimbizi kutoka nchini Burundi waishio Tanzania mkoani Kigoma katika kambi ya Nduta Wilayani Kibondo  waanza kurejea nchini kwao leo hii ikiwa ni makubaliano kati ya serikali ya Tanzania na Burundi.
Wakimbizi 302 ndio walio rejea siku ya leo ikiwa ni awamu yakwanza ya kampeni ya kuwarejesha wakimbizi takribani elfu12 kufikia mwishoni mwa mwaka huu wa 2017.
Wakimbizi hao wamesafirishwa kwa kutumia usafiri wa mabasi mpaka nchini Burundi, Tanzania imekua ni nchi inayohifadhi wakimbizi wengi kutoka Burundi na Kongo kuliko nchi nyingine katika ukanda wa Afrika mashariki.
Kwa mjiu wa taarifa ya shirika la wakimbizi duniani UNHCR iliyotolewa mwezi juni, kufikia wakati huo kulikua na wakimbizi 241,000 kutoka nchini Burundi  huku asilimia 60% ya idadi hiyo ikiwa ni watoto

Chapisha Maoni

0 Maoni