Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MBUNGE WA GEITA AACHIWA KWA DHAMANA




Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi( CCM)  Mkoani Geita ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Geita,Joseph Musukuma na madiwani nane wa halmashauri mbili za wilaya ya Geita wapo nje kwa dhamana baada ya kusota rumande kwa takribani siku sita.

Viongozi hao walipandishwa kizimbani leo Septemba 19, Mahakama ya Hakimu mkazi mkoani Geita,wakikabiliwa na makosa manne,Ikiwemo kufanya mkusanyiko usio halali na kufunga barabara inayoelekea mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) hivyo kupelekea kiasi cha wafanyakazi wa machimbo hayo kushindwa kufika kazini.

Washitakiwa wote wamekana kutenda makosa hayo na kesi hiyo imeahirishwa mpaka itakapoitishwa tena Oktoba 10, Mwaka huu.

Chapisha Maoni

0 Maoni