Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MSANII DARYO PRINCE AWASHAURI WASANII CHIPUKIZI



     
 Daryo Prince ni msanii wa bongo flava mzaliwa wa  jiji la Daresalaam ambae kwa sasa anatamba na wimbo  unaoitwa nyota yangu ambao ameurekodi katika studio ya US ambayo  makazi yake yaliyopo Ubungo,ambapo amefanikiwa kuufanyia video.
  Wimbo wake wa kwanza amerekodi katika studio ya US  hatahivyo wimbo huo  haukupata kufanya vizuri,akiendelea Daryo ameiambia plan media  sababu iliyopelekea muziki wake  kutopata nafasi ya kufika mbali ni kukosekana kwa kupata nafasi ya kutosha kwenye vyombo vya habari.
  Pia Daryo amemuambia mwandishi wetu kuwa katika kufanya kwake kazi alifanikisha kufanya wimbo unaoitwa acha niende kwa Diamond ambao pia amefanikiwa kuufanyia  video ambayo inachezwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari vilivyopo nchini na kupelekea kupata mafanikio kama vile kuitwa kutumbuiza katika maonyesho mbalimbali.
  Akielezea mipango yake kwa sasa Daryo amesema anakazi inayokuja hivi karibuni ambayo amefanikiwa kufanya na Goodkuck Gozbert ambae ni msanii wa nyimbo za injili anetamba na kibao chake kinachoitwa shukurani.
 vilevile katika ushauri alioutoa juu ya wasanii  chipukizi amewaasa waweke umakini katika kazi zao wanazozifanya ili kuhakikisha wanaendana na kasi ya kibiashara iliyopo kwenye soko la muziki wa bongo flava pamoja na miziki mingine,Pia ameiomba serikali iweke sheria za kulinda mali za wasanii pamoja na kuwachukulia hatua kali wale wote wanao hujumu kazi za wasanii.
 

Chapisha Maoni

0 Maoni