Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MAKUMBUSHO FC YASHIKWA PABAYA.

         
Na.Rashid Mongola.


Siku ya Alhamisi tarehe 12 kulikuwa na mchezo mkali katika uwanja wa Kinesi uliopo ubungo,mechi hiyo ilikuwa ya kirafiki kati ya timu ya Mshikamano ya daraja la kwanza ambayo inafundishwa na kocha Waziri Mahazi ilipambana na timu ya Makumbusho fc iliyopo ligi daraja la tatu ambayo ipo chini ya kocha John Mashaka.
Mchezo huo ulimalizika kwa jumla ya mabao 2 kwa 1 ambapo makumbusho imeonjeshwa kichapo kutoka kwa wapinzai wao ambao wanashiriki ligi daraja la kwanza.Mshikamano fc ilipata ushindi huo baada ya mchezaji Ali Kabunda kupiga shuti kali dakika ya 32 na kufanya waongoze kipindi cha kwanza kwa goli ,oja.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kushambuliana kwa zamu huku Makumbusho wakionekana kuamka kwa kasi kwenye dakika ya 75 na kuchomoa bao na kufanya mchezo kuwa mkali Zaidi,katika muendelezo wa mashambulizi timu zote zikitafuta ushindi hatimae Wilson Wilege aliihakikishia timu yake ya Mshikamano ushindi kwa kupiga bao zuri katika dakika ya 85 na kufanya mchezo kumalizika 2-1.
Baada ya mchezo huo muandishi wetu alifanikiwa kuwahoji makocha wa timu zote mbili,kwa upande wa kocha John alisema mchezo ulikuwa mzuri ila kwa upande wake alisema alikuwa akijaribu kikosi,ila imekuwa tofauti kwa kocha wa Msimamo fc Mahazi ambae akiwakilishwa na mshauri wa timu hiyo alisema walikuwa wakijiandaa na mchezo ujao wa ligi daraja la pili dhidi ya Mgmbo jkt ya jijini Tanga.

Chapisha Maoni

0 Maoni