Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MAYANGA ATAJA KIKOSI CHA KUIKABILI BENIN.



NA.RASHID HASSAN
.
KOCHA wa timu ya Taifa ya Tanzania Salumu Mayanga ametaja kikosi kitakacho ivaa timu ya Benin tarehe 11 mwezi wa 11 mwaka huu ambao mchezo huo unatarajiwa kufanyika huko Benin huku Stars ikiwa ugenini katika pambano hilo,mchezo huo utakuwa wa kirafiki baina ya nchi mbili ambapo kwa Taifa stars inaingizo jipya la wachezaji akiwemo Yohana Nkomola na Ramadhani Kabwili.

Kikosi hicho cha stars kinajumuhisha jumla ya wachezaji 24 ambao baadhi yao ni wachezaji vijana chipkizi wanaoinukia kwenye soka,kikosi hicho kinaongozwa na;Goliki[pa,Aishi Manula,Peter Manyika na Ramadhani Kabwili,Ulinzi unaongozwa na,Kelvin Yondani,Boniphas Maganga,Abdi Banda,Gadiel Michael,Nurdin Chona,Erasto Nyoni na Dickson Job.

Viungo wanaongozwa na Himid Mao,Hamis Abdalah,Mzamiru Yassin,Shiza Kichuya,Raphael Daud,Simon Msuva,IbrahimAjib,Mohamed Issa,Farid Mussa na Abdul Mohamed,huku nafasi ya ushambuliaji ikikamatwa na Mbwana Samatta,Mbaraka Yusuph,Elias Maguli na Yohana Mkomola.


Chapisha Maoni

0 Maoni