Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

WAZIRI MKUU WA UHISPANIA AVUNJA BUNGE LA CATALONIA

Waziri mkuu wa Uhispania Mariano Rajoy, amevunja bunge la Catalonia na kuitisha uchaguzi wa mapema ili kurejesha hali kawaida katika eneo hilo.
Mapema Bunge la Catalonia lilipiga kura kujitangazia uhuru kutoka Uhispania.
Hatua hiyo iliungwa mkono kwa kura 70 -10 kura ambayo ilisusiwa na wabunge wa upinzani.
Waziri mkuu wa Uhispania Mariano Rajoy, mapema aliwaambia maseneta kuwa udhibiti kamili ulihitajika kurejesha sheria , demokrasia na udhabiti eneo la Catalonia.
Mzozo huu ulianza wakati watu wa Catalonia waliunga mkono uhuru kwenye kura iliyokumbwa na utata mapema mwezi huu.
Serikali ya Catalonia ilisema kuwa asilimia 43 ya watu walioshiriki katika kura hiyo asilimia 90 waliunga mkono uhuru.
Lakini mahakama ya katiba nchini Uhispnaia imeitaja kura hiyo iliyo kinyume na sheria.
Bunge la Uhispania bado halijapiga kura kuamua ikiwa kwa mara ya kwanza litatekeleza kipengee cha 155 ya katiba ambacho kinairuhusu serikali kuchukua hatua zifaazo dhidi ya eneo lolote ikihitajika.
Itairuhusu Uhispania kuwafuta kazi viongozi wa Catalonia na kuchukua udhibiti kwa uchumi wa eneo hilo, polisi na vyombo vya habari vya umma.




SOURCE. BBCSWAHILI.COM

Chapisha Maoni

0 Maoni