Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

BAISA, NAMPENDA IRENE UWOYA

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Muimbaji wa nyimbo za injili Tanzani Baisa Mhela amelezea  kuwa post yake katika akaunti yake ya instagram kuwa siyo kiki na badala yake alikua anampa pole kipenzi cha moyo wake Irene Uwoya kwa kumpoteza mme wake wahalali  Ndikumana.

Siku kadhaa zilizo pita mala baada ya Irene Uwoya kumpoteza mme wake wazamani Ndikumana, Baisa aliandika maneno haya kupitia akaunti yake ya instagram “Kwa kweli nakupa poleee sana  @ireneuwoya8 Kwa kupotelewa na mme wako wa halali #ndikumana Kama bible inavyosema kwenye 1korinto 7:9+ yapaswa sasa uolewe kihalali na bible inaruhusu naomba uliweke moyoni jambo hili nakusubili upate amani ya moyo tufunge ndoa iliyo halali achana nao hao #ubongowaflavour Walikuharibu mpaka kubadili dini  njoo sasa tufunge ndoa achana na huyo mhuni @dogojanjatz   Njoo tudumishe pendo halisi nilikuota naona nafasi yangu imefika sasa baada ya kupoteza ndikumana wako   Njoo nisaidie kulea mwanangu #reneebaisa” mwisho wa kunukuu.

Baisa hakuishia hapo alipost video inayo muonesha Irene uwoya akiwa analia huku ukisikika wimbo wake Baisa Mhele unaofahamika kwa jina la #Usilie jambo ambalo liliibua hisia tofautitofauti kwa wadau wa muziki wa ijili ndipo plan media iliamua kumtafuta Baisa
.
Aidha amesema kuwa anampenda Irene Uwoya na ni vibaya kwa mkristo alie okoka kuelezea hisia zake kwa mke wa mtu ila kwa wanandoa wowote wanaruhusiwa kuoa baada ya mmoja wapo kufa na ndiyo maana ameamua kuweka hisia kwa uwoya baada ya kutimiza kipengele hicho.

Vilevile Baisa amesema yupo katika mazungumzo na Irene Uwoya mengine mashabiki wake wataendelea kuyajua atakapo yaweka wazi baada ya uwoya kumruhusu kufanya hivyo maana hawawezi kuropoka zaidi ya yate wasubirie mambo mazuri.

Pia Baisa amesema kuwa watanzania waache dhana ya kusema kila jambo kuwa ni kiki kwasababu siku hizi hata mtu anapo mpenda mtu imekuwa ni kiki na badala yake watambue kila mtu anahaki ya kumpenda mtu wa hadhi yeyote.


Baisa amemalizia kwa kusema kuwa ameokoka anampenda Yesu ni kijana ambae bado hajaoa  na anatarajia kuo mapema  mwakani na mlengwa wake atatimiza agano hilo  kwa kadri atakavyo ongozwa na Roho mtakatifu pia amewaomba mashabiki wake kumuombea mipango yake  ikamilike mapema aweze kumleta ndani Irene Uwoya.

Chapisha Maoni

0 Maoni