NA.
GOODLUCK CHRISTOPHER
Katika
ufugaji wa kuku mtuji wa kuanzia huwa ni tatizo kubwa sana hasa pale mtu anapo
tembelea miradi mbalimbali ya watu wanao fuga kuku hao na wanapo jaribu kuuliza
mtaji walio anza nao wanaogopa kwa kutajiwa mtaji mkubwa.
Siyo
lazima wewe kuanzisha mradi Mkubwa kama unayo iona ya wengine. Hao mpaka
kufikia hapo wamechukua muda kidogo na wamekutana na changamoto nyingi na hizo
ndizo zime wafikisha sehemu hiyo unayo iona.
Hivyo
hata kwa mtaji mdogo kabisa unaweza kuazisha mradi wako wa ufugaji wa kuku na baada ya muda nawewe utakuja
kutembelewa katika mradi wako.
Katika
ufugaji kuku kuna aina nyingi za kuku Leo tuangalie ufugaji wa kuku wa nyama [broiler].
Hivi
ni vitu vya msingi na vya kuzingatia unapo hitaji kufuga kuku wa nyama [broiler]
hivyo lazima uzingatie haya ili kufuga kuku ambao watakuletea faida kubwa
pasipo kukuingizia hasara katika ufugaji wako.
Ø Eneo, Upate eneo lenye hewa ya kutosha namwanga wa kutosha na
joto la wastani ambalo ni rafiki kwa kuku hao kuishi
Mtaji, Lazima uwe na maji ya kutosha ambayo ni safi na salama
kwa sababu kuku nao wanahitaji maji ya kutosha.
Banda, Lazima uwe na banda ambalo ni safi na lenye ukubwa wa
kuweza kuishi idadi ya hao kuku unao hitaji kufuga maana likibana sana watakufa
wote.
Vifaa, Lazima uwe na vifaa vya kutosha vya kuwawekea chakula
na maji na vya kufanyia usafi ndani ya banda la kuku hao
Chakula, Hakikisha unawapatia chakula cha kutosha marakwamara
ili wakue haraka na wenye na afya nzuri
.
Dawa, Hakikisha unawapatia chanjo marakwa mara ili kuwakinga
na magonjwa mbalimbali yanayo weza kuhatarisha uhai kuku hao
Hayo
ndio mahitaji kwa kuku wa nyama [broiler] hapa Leo hatuta ongelea hayo
mahitaji, tutaongelea gharama za matunzo kuanzia kununua vifaranga hadi
kuuza na faida yake ipoje! Kwa kawaida watu hujua kufuga kuku ni mpaka uwe na
mtaji Mkubwa lakini siyo hivyo, Hata mtaji wa Laki 5 unaweza fuga kuku [broiler]
na ukapata faida nzuri na jinsi utakavyo endelea kufuga mtaji wako
utaendelea kukuwa zaidi.
Hapa
tunaanza kwa mtaji mdogo wa kuanza na vifaranga 100
Kuna
makapuni mengi yanauza Vifaranga. Kuna bei tofauti tofauti sh 1300 . sh 1400.
Sh 1500.
Kwahapa
tuna tumia Vifaranga wa bei ya sh 1400
Utanunua
kifaranga kimoja 1400×100=140000
Siku
umeenda kuchukua sasa unatakiwa huku nyuma uwe umekamilisha yafuatayo,
Banda
umelisafisha vizuuri, na unatenga kona moja ambayo utaitengenezea umbo la nusu
duara (brooder) ndani ya brooder kutakuwa maranda pia weka magazeti
, magazeti husaidia maji ya kimwagika utaweza kusafisha kiurahisi bila kusahau
vyombo vya chakula na maji , chanzo cha joto unaweza tumia jiko la mkaa,
balbu chungu au taa ya chemli.
CHAKULA
Vifaranga
100 kwa wiki 4 au 5 unaweza tumia mifuko 5 ya kg 50 mpaka kuuzwa.
Wiki
Mbili za mwanzo
Starter
mash mfuko mmoja sh 60000 kwa mifuko miwili . 60000×2=
Sh
120000=
Wiki
ya Tatu.
Growers
pellet mfuko mmoja 73,000/=.
Wiki
ya 4
Finisher
mash 57,000/= 57000×2=114000.
Jumla
Sh
114000+73000+120000+140000=
Sh
447000
Dawa
na kununua maranda ingharimu sh 53000.
Kwahiyo
kwa matunzo hadi kuuzwa watagharimu sh 500000.
Katika
kuuza kuku mmoja sh 6000 × 100= Sh600000.
Faida
ni sh 100000 kwa mwezi mmoja, utakavyo endelea kufuga mtaji wako
utaongezeka. Na utazidi kuwa mzoefu katika ufugaji wa kuku[broiler]. Pia bei ya
chakula hutofautiana hii bei niliyoitumia ni hii baada ya chakula kupanda ila
kuna sehemu chakula mfuko wa kg 50 inafika hadi sh 51000-54000..
Pia
sio utasimamisha shughuli zako zote kwa ajili ya kuku.
Vitu
vya kuzingatia kabla ya kuanza kufuga, chunguza kwanza soko lao lipoje kwahapo
ulipo ili utakavyo wafuga kwenye kuuza wasije wakasumbua kuuza.








0 Maoni