NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Ukiachana na Blazil Tanzania ni nchi yapili kwa kuongoza na
vivutio vingi dunia na mapamgo ya ambani ni moja kati ya vivutia vinavyo
patikana hapa nchini Tanzania, mapango hayo yanapatikana kasikazini mashariki
mwa Tanzania katika mkoa wa Tanga
.
Vilevile mkoa wa Tanga ni moja kati ya mikoa iliyo barikiwa
na vivutio vingi vya utali ikiwemo chemichemi ya maji moto lakini leo hii
hatuto zungumzia kivutio kingine bali
tutazungumzia mapango ya amboni nikukaribishe sana katika makala hii fupi
ambayo utapata kujione maajabu ya mapango hayo.
Mapango ya Amboni yaligunduliwa karne ya 16,taarifa
zilizopo ni kwamba watu wa makabila yaliyoishi jirani na eneo hilo,
Wadigo,Wasambaa,Wabondei na Wasegeju,walikuwa wakiyatumia kwa ajili ya
matambiko ya mizimu tangu Karne ya 16.
Eneo la Mapango hayo wakati huo lilijulikana kwa jina la
Mzimu wa Mabavu,Watu kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya Tanga, mpaka leo
hii hufika mapangoni hapo kwa ajili ya kutambika.
Kampuni ya wazungu ya
Amboni Limited,iliyokuwa ikimiliki mashamba ya Mkonge katika mkoa wa
Tanga,ilimiliki eneo hilo la mapango mwaka 1892,ili kulitumia eneo hilo kama
sehemu ya kupumzikia.
Serikali ya Tanganyika ilianza kutangaza eneo la mapango
hayo kuwa eneo la hifadhi mwaka 1922,baada kujulishwa mapango hayo na wamiliki
wa Amboni Limited.
Mwaka 1937 Serikali ilipitisha Sheria ya mambo ya kale
(Monuments preservation ordinance of 1937) iliyofuatiwa na ile ya mwaka 1953
ambayo imesaidia kulinda mambo ya kale.
Mapango hayo yalitokana na mabadiliko ya nguvu za asili
,zilizobadilisha maumbile ya miamba ya chokaa kipindi cha Jurasiki (Jurassic
period) miaka milioni 150 iliyopita.
Kulingana na utafiti uliofanywa, eneo hilo la
Mapango,lilikuwa chini ya maji miaka milioni 20 iliyota, na linakadiriwa kuwa
na ukubwa wa kilomita za mraba zisizo pungua 234,lenye mazingira ya uoto
wa asili.
Utafiti uliofanywa Mturi (1975) njia ya kwanza ni ya maji ya
Mvua yanapochanganyika na hewa ya [Carbondioxide] katika anga na kutengeneza
tindikali ya kaboni (Carbonic acid) ambayo inauwezo wa kuyeyusha madini ya
Calcium Carbonate yanayounda sehemu kubwa ya miamba ya chokaa.
Maji hayo yenye tindikali husababisha mabadiliko
yanapoteremka kuelekea aridhini,yafikapo aridhini meza ya maji (Water Table) na
yakiendelea kuongezeka,maji hayo yenye tindikali huwa na uwezo wa kuyeyusha
maungio ya miamba,na sehemu laini zaidi za miamba na kusababisha nyufa.
Nyufa hizo huzidi kupanuliwa na maji yanayotembea na
kusababisha baadhi ya mawe kuporomoka na kufanya mapango, kasi ya maji
inapozidi njia ndogondogo hupanuliwa na kuwa kubwa zaidi,na inawezekana mapango
madogo madogo kuunganishwa na hatimaye kuwa na mfululizo wa mapango ya aina
tofauti tofauti.
Zifuatazo ni baadhi ya picha zinazo onesha maajabu yaliyopo katika mazpango hayo na hapa tuaanza na mlango wa kuingilia ndani ya mapango hayo.
Hapa ni njee katika mlango wa kuingilia katika mapango haya na pichani ni mtalii wandani Goodluck Christopher.
Pichani hili ni eneo ambalo hutumika kwa ajiri ya matambiko, watu hutokea maeneo mbali mbali na kuja kufanyia matambiko kaika eneo hili.
pichani ni eneo linalo fananishwa na mlima kilimanjaro, na unao waona pichani ni watali wa ndani kutoka chuo cha uandishi wa habari [TSJ] DSM.
Pichani ni sehemu inayo fananishwa na myama jamii ya paka [CHUI] akiwa amelala.
MWAMBA unaokua na kuongezeka hasa katika kipindi cha
Mvua,kutokana na mabadiliko ya kikemikali katika miamba ya Chokaa,inaongezeka
kwa kiasi cha milimeta 7 katika kila miaka 100.
NJIA nyembamba iliyopo ndani ya Mapango,Conrad Fidelisi mtalii wandani akiwa anapita kwa tabu katika njia hiyo.
MWAMBA unaoonyesha Matiti YA mwanamke,ambao ni miongoni mwa vivutio vya watalii wa ndani na nje ya nchi.
BAO la kete ambalo lipo umbali wa futi 15 kwenda juu ya pango,ambapo watalii wengi huvutiwa na sehemu hii,ambapo Baba wa Taifa alikuwa shabiki mkubwa wa mchezo wa bao.
KOCHI (Sofa) la jiwe ambalo limo ndani ya Mapango ya
Amboni, Goodluck na Sarafina wakiwa wamekaa katika Sofa hilo ambalo lipo katika kituo
namba nne (4) kilichopo ndani ya mapango.

Huu ni mwamba uliojichonga ukawa kama msikiti na kuna maneno ya kiarabu kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Quroan.

Huu ni mwamba ambao umejichonga kama sanamu ya bikra maria pamoja na kitabu kitakatifu cha Biblia hivyo hufananishwa na kanisa.

Huu ni mwamba ambao umejichonga kama mnara wa marekani ambao ni maarufu sana kwenye maigizo ya kimarekani mara tu yanapo anza na jina la "CUROMBIA"

Huu ni mwamba wenye sura kama meli ambayo imetia nanga bandarini hatika sehemu ya chini.

Huu ni mwamba wenye sura ya ndege inayo beba abiria kukiwa kuna ngazi ya kupandia, mlango wa kuingia ndani kama inavyoonekana hapo pichani.

Hili ni jiwe lenye mfanano na makalio ya binadamu kama inavyoonekana pichani.

Huu ni mzizi wa mti ulio ingia ndani ya pango na kutengeneza alama ya mshale unao elekea kwenye mlango wa kutokea, kama mtu amepotea njia ndani ya pango anapo uona mzizi huo unaweza kumsaidia na kuikumbuka njia ya kutokea.

Huu ni mwamba uliojichonga ukawa kama msikiti na kuna maneno ya kiarabu kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Quroan.

Huu ni mwamba ambao umejichonga kama sanamu ya bikra maria pamoja na kitabu kitakatifu cha Biblia hivyo hufananishwa na kanisa.

Huu ni mwamba ambao umejichonga kama mnara wa marekani ambao ni maarufu sana kwenye maigizo ya kimarekani mara tu yanapo anza na jina la "CUROMBIA"

Huu ni mwamba wenye sura kama meli ambayo imetia nanga bandarini hatika sehemu ya chini.

Huu ni mwamba wenye sura ya ndege inayo beba abiria kukiwa kuna ngazi ya kupandia, mlango wa kuingia ndani kama inavyoonekana hapo pichani.

Hili ni jiwe lenye mfanano na makalio ya binadamu kama inavyoonekana pichani.

Huu ni mzizi wa mti ulio ingia ndani ya pango na kutengeneza alama ya mshale unao elekea kwenye mlango wa kutokea, kama mtu amepotea njia ndani ya pango anapo uona mzizi huo unaweza kumsaidia na kuikumbuka njia ya kutokea.
Hili ni pango la jinsia ambalo linaonesha picha zinazo fananishwa na jinsia ya kike na ya kiume za binadamu
Huu ni uoto wa asili unaopatikana nje ya mapango hayo.
Na huu ni mwisho wa makala yetu kwaleo ambapo tulikua tukizungumzia maajabu yaliyomo kitika mapango yaambani ambayo pia ni kivutio kikubwa cha utalii katika nchi yetu ya Tanzania ambapo watalii wa ndani na nje hutembelea mapango hayo na kuyashuhudia maajabu hayo yaliyomo, kumbuka kuwa hayo yalikua baadhi ya maajabu yayo patikana ndani ya mapango hayo panapo majaliwa tutakuletea maajabu mengine endelea kutufatia kupitia kituo chako pendwa cha plan media.
Na huu ni mwisho wa makala yetu kwaleo ambapo tulikua tukizungumzia maajabu yaliyomo kitika mapango yaambani ambayo pia ni kivutio kikubwa cha utalii katika nchi yetu ya Tanzania ambapo watalii wa ndani na nje hutembelea mapango hayo na kuyashuhudia maajabu hayo yaliyomo, kumbuka kuwa hayo yalikua baadhi ya maajabu yayo patikana ndani ya mapango hayo panapo majaliwa tutakuletea maajabu mengine endelea kutufatia kupitia kituo chako pendwa cha plan media.
SHUKRANI ZA PEKEE ZIMUENDEE KILA ALIE WEZESHA MAKALA HII IKAMILIKE IKIWEMO KELVINI KIGADYE [MPIGAPICHA] NA WENGINE WOTE WALIO SHIRIKI KWA NAMNA YEYOTEILE.














0 Maoni