Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI WAASWA KUIMBA NYIMBO ZAO KATIKA ROHO NA KWELI

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania Bw. Heri Mboya  alifanya uzinduzi wa albamu yake mwishoni mwa wiki iliyo pita inayo fahamika kwa jina la Anajibu maombi , uzinduzi huo ulifanyika katika kanisa la E.A.G.T   Vwawa  Mbugani  wilaya ya Mbozi mkoani  Songwe,  Plan Media imemtafuta Bw.Mboya nae alikua na haya ya kusema “Ninamshukuru Mungu sana uzinduzi ulikua vizuri mno watu waliofika ni mashahidi walimuona Mungu kwa namna ya pekee”.

Aidha Mboya amesema aliamua kufanya uzinduzi huo mkoa wa Songwe kwasababu ni nyumbani aliko zaliwa hivyo aliamua afanyie nyumbani kwanza maana aliona nivyema kuwaonesha matunda mazuri  wale walio mlea kiroho tangia akiwa mdogo.

Vilevile amewaasa waimbaji waimbaji wa nyimbo za injili waimbe nyimbo zao katika Roho na kweli, wakati huohuo  ameviasa vyombo vya habari Tanzania kusaidia muzi huu  kuutangaza kwa nguvu kubwa kama wanavyo fanya kwenye mziki ule wa upande wapili [muziki wa kidunia].

Albamu hiyo ni yakwanza kwake kuizindua iko katika mfumo wa DVD  ina nyimbo nane  ambazo ni Anajibu maombi , Kua uyaone, Nazisubiri, Wasamehe, Nduna , Nimwema , Usilie na Natembea na yesu. Albamu hii bado haijapata msambazaji ukiihitaji anakuletea ulipo kwa mawasiliano nitakayo weka hapo chini.

Pia amewaomba watanzania ambao ni wapenzi na wasio wapenzi wa mziki wa injili kununua albamu hiyo ya Anajibu maombi  maana ni nzuri sana na mtu hata jutia kuinunua na kuendelea kumuunga mkono katika huduma yake,na yuko tayari kwa mialiko anahudumu sehemu yeyote kwa utukufu wa Mungu.

Hata hivyo amesema matarajio yake makubwa ni kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji na kwa nguvu zake zote kingali akiwa kijana na akiwa bado ana nguvu za kutosha kumtumikia Mungu wa mbinguni alie hai.

MAWASILIANO YA BW. HERI MBOYA

WhatsApp  : 0655 174 178  na kumpigia kawaida

Facebook  :  @Heri Mboya

Instagram  :  @mboyaheri

PICHA ZA HERI MBOYA AKIWA KWENYE UZINDUZI HUO SIKU YA IJUMA MOSI TAREHE 25/11/2017
 







TUNAOMBA RADHI KWA MUONEKANO HAFIFU WA PICHI HIZO HAPO JUU ZINAZO MUONESHA HERI  MBOYANA WACHEZA SHOO WAKE  AKIIMBA KATIKA UZINZUZI HUO MWISHONI MWA WIKI ILIYO PITA.



HIZI NI PICHA BW. HERI ALIZOPIGA NA WENZAKE NJE KIDO YA KANISA LA E.A.G.T VWAWA MKOANI SONGWE ALIPO FANYIA UZINDUZI HUO.



Chapisha Maoni

1 Maoni