Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

POLISI BARABARANI, WATAKIWA KUPANGA UTARATIBU MAKINI




Image result for askari wa barabarani


                 
NA.RASHID HASSAN


WATUMIAJI wa magari yanayotoa huduma ya usafiri  jijijni Dares-salaam[dladala]waliomba jeshi la Polisi wa barabarani kuwa makini na muda pamoja na kupanga mikakati sahihi na madhubuti itakayo okoa muda wa watumiaji wa usafiri pamoja na kusaidia ongezeko la uchumi wa taifa letu. 

Wakiongea mwandishi wa gazeti la Raia Tanzania kwa nyakati tofuti wasafiri hao wa daladala wamesema ya kuwa kwamba kumekuwa na tabia ya kusimamishwa kwa magari ya abiria mara kwa mara na wkati mwingine huchukua takribani robo saa kwa askari hao kumaliza ukaguzi wa basi.

Mmoja wa watumiaji wa daladala hizo aliejulikana kwa jina moja la Besha amesema kumekuwa na utaratibu usio faa na ambao hauzingatii muda wa wasafiri kwani huchelewesha watu waendao makazini vilevile hupelekea kupunguza ama kuchelesha mizunguko ya ruti kwa wafanyakazi wa mabasi hayo na mwishowe kukosa kipato cha kuridhisha.

Vilevile mwandishi wa gazeti hili alipata kumhoji mmoja wa Dereva wa daladala zifanyazo safari zake Gongo la Mboto Makumbusho ambae hakupenda jina lake lifahamike alisema kuwa ni kweli wanakuwa na makosa katika mabasi yao lakini tatizo ni pale wanapokuwa wanakamatwa mara kwa mara na askari tofauti jambo ambalo hakubaliani nalo na badala yake ameliomba jeshi la polisi kuweka utaratibu sahihi wa kudhibiti magari mabovu.

Ikumbukwe kuwa mapema katika uongozi wa awmu ya tano umewekwa utaratibu mzuri ambao unatumiwa na jeshi la polisi wa barabarani,ambao utaratibu huo ni wa kumuandikia kosa pamoja na kulipia kupitia max malipo,ambapo utaratibu huo ni mzuri na umesaidia kutunza muda kwa watumiaji wa usafiri wa daladala.

Chapisha Maoni

0 Maoni