Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

SABABU ZINAZO WAFANYA WAIMBAJI WACHANGA KATIKA MUZIKI WA INJILI KUTO KUJULIKANA

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania Bw.Mecracy Bukulu amesema kuwa sababu kubwa inayo wafanya waimbaji wachanga wa nyimbo za injili Tanzania  kuto kujulikana kuwa ni udhamini  katika nyimbo hizo kuwa mdogo ukilinganisha na muziki wa upande wa pili yani bongo freva.

Aidha Bukulu amesema  kuwa mbali na waimbaji hao kujulikana makanisani  kwao inakua changamoto kubwa kujulikana sehemu kubwa kwasababu walio wengi hawana pesa yakutosha kutangaza huduma yao nje ya makanisa wanayo Sali kwa maana ya kutumia vyombo vya habari pamoja na matamasha mbalimbali na hatimae wanaishia kujulikana ndani ya makanisa wanayo Sali.

Vilevile Bukulu amesema  kuwa wasambazaji wa nyimbo za injili Tanzania ni wachache ukilinganisha na idadi ya waimbaji wa nyimbo hizo kwasasa, hivyo wanawatoza gharama kubwa kuzisambaza nyimbo hizo jambo ambalo waimbaji wachanga hushindwa kumudu gharama hizo.

Pia Bukulu amewaomba watu wenye uwezo na makampuni kuwekeza katika kasambaza kazi za waimbaji wa nyimbo za injili pamoja na kudhamini katika matamasha mbalimbali kama ilivyo katika muziki wa upande wapili yaani bongo freva lengo ikiwa ni kuitamgaza injili kamili ya Yesu kristo kwa watu wote.


Bukulu amemalizia kwa kutambulisha wimbo wake mpya ambao uko katika mfumo wa audio inayo inayo itwa Yesu ni mzuri “Natambulisha wimbo wangu mpya [audio] ya Yesu ni mzuri na imeanza kupokelewa vema na wasikilizaji wa media za gospel Tanzania” mwisho wa kunukuu.

Chapisha Maoni

0 Maoni