Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

BOMOA BOMOA YAIKUMBA TANESCO DAR ES SALAAM

NA .GOOGLUCK CHRISTOPHER

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. Joseph Magufuli ameagiza jengo la makao makuu ya shirika la kuzalisha umeme Tanzania [TANESCO] lililopo jijini ni Dar es salaam kuwekewa alama ya ‘X’ kuashiria jingo hilo kubomolewa, Rais ameyasema hayo katika ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa barabara katika eneo la Ubungo.

Aidha Rais ameongeza kwa kusema kuwa Jengo jingine ambalo litaathiriwa na agizo hilo ni jengo la wizara ya maji ambalo lipo jirani na jingo hilo la shirika la kuzalisha umeme Tanzania TANESCO katika ineo hilo la Ubungo..
 Vilevile Raisi ametoa agizo hilo kutokana na majengo hayo kujengwa  ndani ya hifadhi ya barabara, Zoezi la bomoa boma limekuwa likiendelea, ambapo majengo pembezoni ya barabara inayounganisha mji wa Dar es salaam na maeneo mengine ya nchi yameathirika. Wakaazi wengi waliokuwa wakiishi katika maeneo yanayodaiwa kuwa katika hifadhi ya barabara wamepoteza makazi yao.


Chapisha Maoni

0 Maoni