Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

GEMBE AZUNGUMZIA SABABU ZA WAIMBAJI BINAFSI WA NYIMBO ZA INJILI KUKIMBIA KWAYA

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Mratibu wa kwaya ya vijana kanisa la [KKT] ushirika wa Hananasifu jijini Dar es salaam Bw. Hemeid Msairi Gembe ameeleza sababubu zinazo wafanya baadhi ya waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania  kukimbia vikundi vya uimbaji makanisani maalufu kama Kwaya kuwa ni masirahi binafisi.

Aidha Bw. Gembe ameieleza Plan Media kuwa ubinafsi  umewatawala baadhi ya waimbaji wa nyimbo za injili na kujali masirahi binafsi kwasababu ukifuatalia waimbaji wa nyimbo za injili wanao fanya vizuri chimbuko lake walianza kwenye kwaya lakini baada ya kufanikiwa wanasahau waliko anzia.

Vilevile Gembe amesema waimbaji wengi wanapo zindua albam fedha yote inaingia mfukoni mwao huku kwaya ikizindua albamu fedha inaingia katika mfuko wa kwaya ili kuendeleza huduma katika sehemu mbalimbali hii huwafanya waimbaji kuona kuwa hawafanikiwi na huduma hiyo.

 Gembe ameongeza kwa kusema kuwa muimbaji akishaweza kuimba na kuandika mashairi ya nyimbo hizo za injili anaenda kurekodi wimbo wake binafisi na kusema hili ni jambo jema lakini wimbo huo ukifanya vizuri ndo haonekani tena kwenye kwaya na ukimuuliza atakwambia huduma imembana.

Pia Gembe amesema unakuta waimbaji wa kwaya wanapo hitajika wanatumia gharama zao wenyewe mpaka kumaliza huduma lakini waimbaji baadhi yao huwa wana gharamiwa hivyo huona kwamba hii ni njema kwake hivyo wanasahau kuwa wanapoteza maana ya kumtumikia Mungu wanapo fanya hivyo.

Hata hivyo Gembe amesema kuwa hii inasababishwa na waimbaji wenyewe kutokuwa na misingi mizuri ya neono la Mungu ndani yao hivyo  wanakosa kuwa waaminifu kwa Mungu kwasaba neono la Mungu linasema “Fedha na Dhahabu vyote ni mali ya Bwana” na kama wakimtumikia kwa uaminifu basi  hivyo vitakua vyao.

Vilevile Gembe ametoa ushauri kwa waimbaji wa nyimbo za injili kusoma neon la Mungu kwa wingi waache kusoma mstari mmojammoja na badala yake neono kwasababu Biblia kitabu kinacho jieleza vyakutosha sana  na wasiwe watu wenye tamaa ya pesa  na wakumbuke kuwa tamaa ni dhambi.

Vilevile ameongeza kwa kusema wasigeuze uimbaji kama biashara  kwasababu waimbaji wana nafasi kubwa ya kuwavuta watu kutoka kwa shetani kuja kwa Yesu na kama waimbaji wakizingatia hilo na Mungu atanafungulia baraka juu yao.

Pia Bw.Gembe amemaliza kwa kusema mbali na kumtangaza kristo kwaya yao wameamua kuwa wajasiliamali kwa kuzalisha bidhaa kama Sabuni za kufuria, Dawa za chooni  pamoja na Pilipili ambazo huwasaidia waimbaji wasio kuwa na ajira kuziuza bidhaa hizo na kupata pesa za kujikimu kimaisha jina la kampuni ni “SHUJAA MWENYE NGUVU”


Kujipatia bidhaa hizo za “SHUJAA MWENYE NGUVU”

 Piga simu namba : +255 717 461 193


Kwa picha zaidi za bidhaa zinazo zalishwa na kampuni ya shujaa mwenye nguvu 





Chapisha Maoni

0 Maoni