Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

HERI AELEZA KUJA NA KUPOTEA KWA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Muimbaji na mwandishi  wa mashairi ya nyimbo za injili Tanzania Bw. Heri Mboya ameeleza sababu zinazo sababisha waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania kuja kwa kasi wanapoanza huduma hiyo na kupotea kwa muda mfupi na wengine kupotea moja kwa moja katika huduma hiyo ya kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji.

Aidha Bw. Mboya ameieleza plan media kuwa wengi wao hupoteza ladha ya muziki wa injili na kuiga miziki ya kidunia “Tabia hii inawafanya wengi wasikike kidogo tu harafu wanapotea na mifano tunayo wazi kabisa, Miziki hii ya kidunia hasa hii inayo itwa ya kisasa haidumu zaidi ya mwezi yaani msanii wa bongo freva anaweza akatoa wimbo leo ndani ya mwezi huohuo wimbo unachuja. Sasa muimbaji wa nyimbo za injili kama nae akiiga huko  unataka tutegemee nini kama si kupotea ndani ya muda mfupi?”

Vilevile Bw. Mboya amesema kwamba waimbaji wengi ni wasanii na siyo waimbaji hivyo mtu ambae ni msanii hata utunzi wake wa mashairi ya nyimbo huwa hawamshirikishi  Roho mtakatifu na badala yake wanatumia akili na ujanja wao hivyo wimbo wainjili kama hauna uvuvio wa Roho mtakatifu hauwezi kudumu.

Mboya ameleza kuwa hivi sasa kuna ushindani mkubwa kwasababu waimbaji ni wengi sana hivyo ili muimbaji aweze kuendelea vizuri ni lazima awe  anamshirikisha Mungu katka kila afanyalo ili aweze kumsaidia awe na nyimbo nzuri, waimbaji wengi hawasomi neono la Mungu kwa wingi hili husababisha kuimba nyimbo ambazo hazina ubora zinazo sababisha waimbaji hao kupotea.

Pia amesema kuwa sababu nyingine ni matangazo ya muziki huo kuwa changamoto kwa waimbaji hivyo waimbaji hasa chipukizi wanashindwa kumudu gharama za kuutangaza muziki wao  kupitia vyombo mbalimbali vya habari  ikizingatiwa kuimbaji hao wanashindwa kulipa gharama hiyo hivyo hilinalo linasababisha waimbaji wachanga kuja na kupotea.

Vilevile Mboya amesama kuwa kiburi,Ujeuri, Majivuno  pamoja na kutangatanga hii huwapoteza waimbaji wengi kwasababu baadhi yao wakisha inuka na kuwa na majina wanainua mabega na kusahau kuwa alie wapandisha ni Mungu, hii humchukiza Mungu hivyo Mungu huwashusha na wanapotea kabisa masikioni mwa watu.

Hata hivyo Mboya ametoa ushauri kwa waimbaji wa nyimbo za ijili Tanzania, Mboya amesema waimbaji wapendane na hii ni kwa wakongwe pamoja na wanao chipukia  kwasababu neno la Mungu linasema “Amri kuu tuliyopewa ni upendo” lakini kwa waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania bado neono hilo halitiliwi maanani “Mungu atusaidie”

Vilevile amewasa waimbaji wawe rohoni na wasiimbe kwa  ajiri ya kuwaburudisha watu pekee hivyo wakumbuke dhima ya nyimbo za injili ni kumtumikia Mungu , Kumsifu na kumuabudu katika Roho na kweli.

Pia Bw. Mboya anawakaribisha kwenye tamasha la uzinduzi wa albamu  yake inayoenda kwa jina la “ANAJIBU MAOMBI” Tarehe 25/11/2017 ni siku ya jumamosi kuanzia saa 1:00 mchana  kanisa la [E.A.G.T] Viwanja vya Mbugani  Mbozi mkoani Songwe, Albamu hii iko katika mfumo wa [DvD/VIDEO] Hivyo usikose kununua albamu hiyo ikiwa na nyimbo zenye upako.   Kutakua na waimbaji kutoka sehemu mbali mbali na kutoka Dar es salaam atakuwepo Emanuel Mbasha pamoja na Matumaini.

Wasiiana na Heri Mboya kwa:
Namba;  0655 174 178

Facebook : Heri Mboya

Chapisha Maoni

0 Maoni