Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

HISTORIA YA BETHA JONATHAN MWAFILOMBE MUIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIIA

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
Betha alizaliwa tarehe 2/2/1996 katika kijiji cha Mababa wilayani Kyela mkoani Mbeya ni mtoto wa saba na wamwisho katika familia ya watoto saba wa mzee Jonathani Mwafilombe, Betha ni muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania pamoja na sauti nzuri aliyo jaliwa ya kuimba pia anauwezo wa kuandika mashairi ya nyimbo za injili kwa maana nyingine ni mtunzi na muimbaji wa nyimbo za injili.

Mnamo mwaka 1997 familia yake ilihamia  Kinondoni shamba  mkoani Dar es salaam kipindi hicho akiwa na umri mdogo umri wa mwaka mmoja, Betha alishi hapo na wazazi wake katika makao mapya  na maisha hayo huku umri ulizidi kusogea.

Mnamo mwaka 2004 akiwa na miaka 8 alijiunga na shule ya msingi Kumbukumbu Kinondoni B, Betha hakubahatika kupata elimu ya awali yaani chekechea na badala yake alijiunga mojakwamoja na darasa la kwanza katika shule hiyo kutokana na umri alio kuwa nao kwa kipindi kile .

Mnamo mwaka 2006 akiwa daresa la tatu familia ilirudi tena mkoani mbeya hinyo ilimlazimu kuhama shule akaomba uhamisho walipo fika mbeya akajiunga na shule ya  wamsingi Mababu katika kijiji cha Mababu wilayani Kyela akaendelea na darasa la tatu akaendelea kupata elimu katika shule hiyo.

Mnamo mwaka 2010 alihitimu elimu ya msingi kwa maana ya  daresa la saba katika shule hiyo ya msingi Mababu hapo alikua na umri wa miaka 16, Betha hakuweza kufanya vizuri katika mtihani wake kitu kilicho fanya wazazi wake kushindwa kumsomesha katika shule binafsi maana kipato chao kilikua hakikidhi kumsomesha katika shule hizo hivyo safari yake ya kielimu iliishia pale.

Mnamo mwaka 2011 Betha aliamua kuokoka katika kanisa la Luthelani[KKT] Mababu mkoani Mbeya na safari yake ya wokovu ilianzia pale ndipo alijiunga na kwaya ya kanisa hilo ambapo alitumika katika kwaya hiyo ndani ya mwaka mmoja.

Mnamo mwaka 2012 alianza kuandika ama kutunga nyimbo zake na kuanza kuingia katika studio ya John Joram  ambapo alipata kurekodi nyimbo tatu ambazo ni 1:Kwa neema  2:Siku za mwanadamu 3: Mambo mengi richa ya kurekodi nyimbo hizo bado alipata changamoto ya ubora wa nyimbo hizo ambao haukuwa mzuri.

Mnamo mwaka 2014 alirudi jijini Dar es salaam huku akiwa na changamoto ya sehemu ili aishi wakati akitafuta studio nzuri, Betha alifanya mawasiliano na mama mkwe wa dadayake ndipo alipo fikia maeneo ya kinondoni shamba jijini Dar es salaam akakubaliwa anaishi hapo.

Mnamo mwaka 2015 Betha alimpoteza babayake mzazi mzee Jonathani  Mwafilombe ilikua tarehe 5/2/2015 ambae alikua akisumbuliwa na tatizo la vidonda vya koo vilivyo pelekea umauti wake jambo hili lilimfanya Betha asikitike kwani babayake alikua ndie nguzo yake katika kila alifanyalo hata hivyo alichukulia tukio lile kama changamoto ya maisha kwakua imeandikwa kila  nafsi itaonja umauti hivyo aliendelea na huduma yake ya uimbaji.

Mwaka huu wa 2017 aliingia katika studio ya Ommary Mkali iliyopo iliyopo Mbezi Ruisi jijini Dar es saam akapata kuboresha nyimbo zile tatu alizo zirekodi kwa John Joram studio mbeya  pamoja na kuongeza nyimbo tano ambazo zinatimiza nyimbo nane kwa sasa  nazo ni 1:Kwaneema,  2: Siku za mwanadamu, 3:Mambo mengi,  4:Hasira hasara,  5:Mali za ulithi,  6:Mwacheni Mungu aitwe Mungu  7:Pigo la mama  8:Ume mwasi Mungu ambazo kwasasa zinafanya vizuri na zinachezwa katika vituo mbali mbali vya radio hapa Tanzania.

Richa ya Betha kuwa muimbaji wa nyimbo za injili pia ni mjasiliamali ambae analima kilimo cha mboga mboga na matunda pamoja na ufugaji wa mifugo aina ya Nguruwe mkoani Mbeya ambavyo humuingizia kipato na kumsadia kufanya shughuli mbali mbali ikiwemo kujilipia gharama za kurekodi nyimbo zake


MAWASILIANO YA BETHA
SIMU. 076 740 265
FACEBOOK.  BETHA J MWAFILOMBE
INSTAGRAM. BETHA J MWAFILOMBE


Huu ndio mwisho wa wasifu wa Betha  Jonathani Mwafilombe tutaendelea kuwaletea wasifu wa watu wengine hivyo usikose kutembelea PLAN MEDIA kwa mambo mengi na mazuri.   Asanteni.

Kama unahitaji kuandikiwa wasfu wako kama Betha wasiliana nasi kwa:
+255713 305 650
planmediatz@gmail.com

Chapisha Maoni

0 Maoni