Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

RAISI AJIHUDHURU TSJOSO

NA. GOODLUCK CHRISTOPHER
  Wakatikati kati ya hao wawili ndie Mh. Fred Peter Iske ambae ameji hudhuru nafasi hiyo kwa sasa picha na Maktaba. Tunaomba radhi kwa muonekano usio ridhisha.

Raisi wa serikali ya wanafunzi TSJOSO katika chuo cha uandishi wa habari Time School of Journalism [TSJ] kilichopo Ilala jijini Dar es salaam Mh. Fred Peter  Isike ajihudhuru nafasi ya uraisi katika chuo hicho leo hii.

Aidha Isike ametoa kauli hiyo katika viwanja vya chuo hicho mala baada ya kipindi cha redio kwa vitendo ambacho hufanyika kuanzia jumatatu mpaka ijumaa saa nane na dakika hamsini mpaka saa kumi kama ilivyo pangwa na uongozi wa chuo hicho.

Vilevile Isike hajatoa sababu mahususi zilizo mfanya kuachia ngazi hiyo na badala yake amesema leo hawezi zungumza chochote kuhusiana na uamzi huo na kuongeza kusema kwamba atabakia kuwa mwanachama wa kawaida katika serikali hiyo ila atazungumzia uamzi huo siku nyingine ambayo hajaitaja.
Kwa upande wa mwalimu mlezi wa wanafunzi chuoni hapo Bw. George Bartazal alipokea uamzi huo kwa masikitiko makubwa na kusema kuwa haijawahi kutokea katika chuo hicho kwa raisi kujihudhuru hivyo imemshangaza sana kuona uamzi kama huo.

Gerge amempongeza isike kwa ujasiri alio uonesha kwasababu ni uamzi mgumu ambao si rahisi kwa mtu mwingine kuufanya  na kusema kuwa kunawatu wengine hulewa na madaraka lakini wengine pia uongozi ni sehemu inayo wafanya wajifunze jinsi ya kuishi na watu.

Pia George amesema kuwa Isike kabla ya kujihudhuru  nafasi hiyo alipokea barua ya kujihudhurukwa kiongozi ikisema kwamba ameamua mwenyewe bila kushurutishwa wala kushauriwa na mtu kuchukua uamzi huo hivyo ameadhimia mwenyewe. 

Aidha George ametangaza kuwa kuanzia leo chuo hicho hakina serikali na badala yake akaamua kutangaza kwa wanafunzi wanao jiona kuwa wana uwezo wa kuwa viongozi kugombea nafasi mbalimbali katika serikali hiyo ambapo kampeni zitafanyika kwa muda mfupi zaidi kwa sababu ni uchaguzi mdogo hivyo haoni haja ya kusubiri  siku 30 za kuitisha uchaguzi huo kwa mjibu wa katiba wakati kuna wanafunzi wanao  tazamia kuanza mitihani hapo Novemba13 na kusema anataka wanao hitimu wasikiache chuo kikiwa hakina serikali .

Vilevile Gerge amewataka wanawake kuamka na kugombania nafasi mbalimbali na si kuwaachia wanaume kugombania nafasi hizo pekee kwasababu wanawake nao wana uwezo mzuri wa kuiongoza serikali hiyo na kutoa msemo huu  “ukiona mafanikio ya mwanaume ujue kuna mwana mke nyuma yake”.

Pia George amemteua Bw. Abdallah Twaha  kuwa mwenyeki wa tume ya uchaguzi uanao tarajiwa kufanyika hivi karibuni na kumuita mbele ya wanafunzi achague kukubali au kukataa kuendesha tume hiyo Twaha amekubali kwa kiapo hiki ‘’mimi Abdala Twaha  kwa heshima niliyo pewa kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi mdogo kwa akili yangu timamu bila kushurutishwa nimekubali’’



Chapisha Maoni

0 Maoni