Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

MAGARI YA KUZOLEA TAKA KITENDAWILI DAR ES SALAAM

NA. MARYAM MMAMBIYA
Wananchi wa Yombo kilakala wilayani Temeke waitaka serikali kuongeza magari ya kuzelea taka , haya yameongelewa na wananch hao baada ya uchache wa magari hayo jambo linalo pelekea mrundikano wa takataka  na kusambaa katika makazi ya watu baada ya sehemu iliyo andaliwa kukusanyia taka kufurika wingi wa taka hizo.

Aidha mmoja wa  wananchi hao Bi. Sabrina Komba ameiambia plan media kuwa ukosefu wa magari hayo unasababisha uchafuzi wa mazingira kwa kiasi kikubbwa  hususa ni katika kipindi hiki cha mvua nyingi ambapo maji hubeba taka hizo na kuzisambaza katika makazi ya watu na zingine huingia katika mto yombo ambapo husafirishwa moja kwa moja mpaka baharini.
Vilevile Bi. Sabrina mesema afya za wakazi hao ziko hatarini kutokana na uchafu huo ambao  unaweza kusababisha magojwa ya mripuko na kupoteza maisha ya wakazi hao hususa ni watoto wadogo wanao cheza michezo yao katika maeneo hayo.

Kwa upande wa mwenyekiti wa mtaa huo Bw.Juma Matari amekiri kuwepo kwa uchafu huo na kudai kuwa  magari yamekua ni changamoto kubwa sana hivyo wapo katika mchakato wa kulitokomeza tatizo hilo na hivi karibuni hali itakua swari na wananchi wataishi kwa amani na afya zao zikiwa njema.

Pia Matari amewata  wananchi hao kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu na kutoa ushirikiano wa hali ya juu kuhakikisha tatizo hilo lina tokomea kabisa ili wakazi waishi katika mazingira masafi na salama kwa afya za wakazi hao.

Hata hivyo suala la usafi wa mazingira limekua changamoto katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam hususa ni katika kipindi hiki cha mvua jambo ambalo linaleta wasiwasi kwa afya za wakazi waishio katika jiji la Dar ea salaam kwa ujumla.


Richa ya mkuu wa mkoa Mh. Paul Makonda kuteua siku ya jumamosi kuwa siku ya usafi katika maeneo yote ya jiji la Dar es salaam siku hiyo imekua haizingatiwi katika baadhi ya maeneo na ndio maana tunaona maeneo mengi yakiwa machafu sana hususa ni katika masoko kama; Buguruni,Tandika, Tandale n.k











Chapisha Maoni

0 Maoni