Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

UHALIFU TISHIO TEMEKE

 NA. MARYAM MMAMBIYA
Wanaichi wa Yombo wilani Temeke jijini Dar es salaam wachoshwa na vitendo viovu wanavyo fanyiwa na kundi la vijana wanao jihusisha na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi,wananchi hao wameiambia plan media kuwa wamekua wakiporwa malizao ndogondogo kama simu,pesa pamoja na mikoba wakati mwingine kuibiwa nguo zilizo anikwa kwenye kamba.

Wakizungumza kwa na plan media kwa nyakati tofauti walikua na haya ya kusema; Bw. Peter John ambae ni mkazi wa eneo hilo amesema huwa anaporwa simu ya mkononi wakati mwingine pesa au viatu na vijana hao nyakati za jioni akitoka katika shughuli zake za kujitafutia kipato
.
Pia Peter ameongeza na kusema kuwa vijana hao wanatumiza zana hatarishi kwa maisha ya binadamu kama visu, nyembe na misumari ambayo hutumia katika kupora mali hizo na mtu anapo nga’ang’ania kuwapa wanavyo vihitaji wana mjeruhi na  zana hizo hivyo watu wengi huwa waoga na kuwapatia vitu hivyo  wanavyo kuwa wakivihitaji vijana hao.

Vilevile mmoja kati ya wavuta bangi  ambae hakupenda jina lake liandikwe amesema kua si kila mtu anae vuta bangi ni mkabaji wa mali ndogondogo bali ni baadhi wasio jitabua wanao fanya hivyo jambo ambalo linafanya jamii iwachukulie hivyo bali wengine wanavuta bangi kwa kujiburudisha kama wengine wanavyo kunywa pombe.

Hata hivyo polisi wamekua wakijitahidi kufanya doria na kuwakamata baadhi  yao na kuwaweka ndani [jera]  baada ya siku kadhaa wanatolewa nje ,richa ya polisi kufanya hivyo bado vijana hao wanaendelea na tabia hiyo ambayo ni kero kubwa kwa wakazi wa eneo hilo.

Pia wakazi hao wameiomba serikali kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo kwakua ni hatari kwa maisha ya wakazi hao  kwasababu lisipo tatuliwa mapema litaathiri kizazi kijacho kwa ujumla hivyo ni vyema kuilitokomeza tatizo kabla halijawa kubwa zaidi.

Tatizo la matumizi ya dawa za kulevya limekua ni tatizo linalo pigiwa kerere na viongozi wakubwa wa serikali na dini lakini bado linaendelea kuwaathili vijana wa kitanzania richa ya kupigiwa kerere kwa kiasi kikubwa pengine elimu inahitajika kwa kiasi kikubwa.

Dawa za kulevya zinapunguza nguvu kazi ya taifa hususa ni kwa vijana ambao ni taifa la leo na taifa bila vijana haliwezi kufika popote wazazi  pamoja na viongozi ni wakati wa kupeana ushirikiano katika kutatua tatizo hili na sio kuwaachia wana siasa hili ni tatizo la kutatua wote kwa ujumla.

Chapisha Maoni

0 Maoni