Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

BAISA AACHIA BARAKA ZA MWISHO WA MWAKA KWA MASHABIKI WAKE.

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Kuekea mwaka mpya muimbaji  wa nyimbo za injili Tanzania anae fanya vizuri kwasasa Baisa  Mhela amekua akiachia video harakaharaka ambapo leo hii ameachia video ya funga mwaka uitwao CHINI YA MSALABA kupitia cha nnel yake ya YouTube @BAISA MHELA, Link yake  bofya hapa>>>> https://youtu.be/vFrMOX3TOblna hii ikiwa ni video ya mwisho ndani ya mwaka huu 2017.

Baisa amesema kuwa sababu za kuachia video harakaharaka sana kwasasa ni kuwapa Baraka mashabiki wake na muziki wa injili kwa ujumla ili kuukaribisha mwaka mpya na mambo mapya.

Aidha baisa amewashukuru mashabiki zake kwa kuutambua mchango wake katika muziki wa injili kwani  ndani ya mwaka 2017 amefanikiwa kukamilisha albam ya DVD yenye nyimbo takribani 7 pamoja na kuingia mkataba na kampuni za mukiziki Tanzania na Kenya kuweka muito kwenye simu [ringtone], lakini pia alifanikiwa kufanya huduma kwenye mikutano na matamasha mbalimbali.

Vilevile Baisa alipitia changamoto mbalimbali ikiwemo kampuni aliyo kua akifanya  nayo kazi mwaka huu kuchelewesha kazi zake ili ziwafikie walengwa lakini pia kurudiarudia baadhi ya kazi kutokana na kazi hizo kukosa ubora.

Pia Baisa amesema hatoweza kuzindua albam ya DVD na badala yake ameamua kutoa video ya wimbo mmojammoja lengo ikiwa ni kuwabariki mashabiki zake pamoja na kuwaanda kupokea kazi nzuri zijazo hapo mwakani pia amewaomba mashabiki kununua nyimbo zake kupitia wasambazaji wake.

Hata hivyo Baisa amemalizia kwa kusema kuwa anatarajia kuachia wimbo wake mpya uitwao JUST  mapema mwakani hivyo amewaomba mashabiki zake kukaa mkao wa kula kuupokea wimbo huo mpya na wenye ubora wa hali ya juu.

WASILIANA NA BAISA MHELA KUPITIA NAMBA 0652 155 399



Chapisha Maoni

0 Maoni