Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

UJENZI WA ZAHANATI KITENDAWILI KISICHO NA JIBU

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Wakazi wa kijiji cha Katete kata ya Mwakizenga wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma wamelalamikia uongozi wa kijiji  kwa kuzorotesha ujenzi wa zahanati unaoendelea katika kijiji hicho huku wakiendelea kupata adha ya vifo kutokana na kutembea umbali wa zaidi ya saa moja kukifuata kituo cha afya cha Mwakizega ili kupata huduma hiyo.

 Aidha Bw.Amri Ibrahim ni mkazi wa kijiji hicho amesema kuwa wanapata tabu sana kuwasafirisha wagonjwa mahututi hususani wamama wajawazito umbali wa kilometa 9 kwa kutumia usafiri wa baiskeli na pikipiki kukifuata kilipo kituo cha afya cha mwakizega.

Kwaupande wake Bw. Mtafiti Mikidadi Amesema kuwa wamekuwa wakichangishwa michango mbalimbali ilikuwezesha ujenzi wa zahanati hiyo lakini mpaka leo hii hakuna mafanikio ya kuendeleza ujenzi wa zahanati hiyo.

Vilevile diwani wa kata ya Mwakizega Bw.Swabiru Basenga amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na hivyo aliamua kufanya mkutano wa hadhara na kuchangia mifuko 30 ya seruji lengo ikiwa ni kuhamasisha wananchi wengine kuchangia ujenzi huo.

Hata hivyo  Basenga amemalizia kwa kusema kuwa alilazimika kuteua nyumba kijijini hapo ambayo inatumika badala ya zahanati pamoja na kuchagua timu ya wataalamu ambayo hufika kijijini hapo mala mbili kwa kila wiki wakati wakisubiria ujenzi huo ukamilike.

Pia wakazi hao wameiomba serikali kuliangalia suala hilo ili kuokoa uhai wa wakazi hao pamoja na maendeleo ya kijiji hicho kwani sera ya nchi inasema kila kijiji kinatakiwa kiwe na zahanati lakini kijiji hicho bado hakijapata zahanati.



Chapisha Maoni

0 Maoni