Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

UJENZI WA SHULE PASUA VICHWA KIGOMA

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Ukosefu wa mwenyekiti wa kijiji kwa muda mrefu katika kijiji cha Katete kata ya Mwakizega wilaya ya uvinza mkoani Kigoma umesababisha kukwama kwa ujenzi wa shule uliokuwa ukiendelea katika kijiji hicho.

Aidha Bw.Amir Juma ni mkazi wa kijiji cha katete amesema kuwa kijiji hicho hakina mwenyekiti na badala yake kijiji hicho kinaongozwa na kaimu mwenyekiti ambae wanaichi hao hawamtambui.

Vilevile Bw.Juma ameongeza kwa kusema kuwa ukosefu wa kiongozi huyo imepelekea kurudisha maendeleo ya kijiji hicho ikiwemo ujenzi wa shule uliokua ukiendele kijijini hapo.

Kwaupande wake Bw. Mtafiti Mikidadi ambae pia ni mkazi wa katete “B”  asema kuwa uongozi wa kijiji hicho wanasema wanalifanyia kazi lakini mpaka leo hii hivyo serikali waliangalie suala hili kwa umakini kwani suala hilo linarudisha nyuma maendeleo ya kijiji hicho.


Pia diwani wa kata ya Mwakizega Mh.Swabilu Mussa Basenga amekiri kuwepo kwa tatizo hilo  na ameshalifikisha kwa mkurugenzi na wanalifanyia utaratibu kuhakikisha wanaanda bajeti ya kufanyia uchaguzi mdogo wa mwenyekiti wa kijiji hicho.  

Chapisha Maoni

0 Maoni