Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

KISA TRANSFOMA,WANAKIJIJI WATESEKA




NA.RASHID HASSAN,

WANAKIJIJI wa  mwandege  chini,katika kata ya Mwandege wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani,wameillalamikia kampuni ya umeme ya Tanesco kwa kitendo cha kuweka Transforma karibu na makazi ya watu jambo ambalo limekuwa likihatarisha maisha ya wanakijiji hicho na kupelekea watu kuzimia,wakati mwingine watoto huweweseka kutokna na milio ya milipuko inayotokea mara kwa mara.

Wakazi hao wakiongea na mwandishi wa plan media wamesema  kwamba wamekuwa wakikosa Amani nyakati ambazo mlipuko wa Transforma hilo unapotokea na kupelekea matatizo kwa wanakijiji hao kama,watoto zao wanashindwa kusoma kwa Amani nyakati za usiku,tatizo la moyo kushuka mapigo yake ama kupanda kwa watu wenye matatizo ya moyo.

Ambapo wanakijiji hao waliwakilishwa na Ndugu  Said Mkawawa,ambaye alisema ni kweli tatizo ni kubwa na wao ndio waathirika wakubwa na amewataka wahusika kuwasaidi haraka iwezekanavyo ili kuwapa Amani ya kuishi pasipo kubugudhiwa na jambo lolote ili kila mmoja afanye jukumu linalomhusu na kwa wakati sahihi.

Katika juhudi za mwandishi wa plan media,alifanikiwa kuongea na mjumbe wa kijiji hicho Bwana[ Ally Hemedi alisema kuwa jambo hilo ni la mda mrefu limekuwa likiwakwaza wanakijiji wake ila juhudi alizotumia ni kubwa ambapo mwanzo lilikuwa nyuma ya nyumba ya mmoja wa wakazi hao lakini baada ya malalamiko limesogezwa mbelekidogo ambapo bado limekuwa ni tatizo kwa wanakijiji hao.

Katika juhudi zilizofanywa na mwandishi wa plan media za kuwatafuta wahusika wakuu wanaolalamikiwa ambao ni Tanesco ya wilaya ya mkulanga zilishindikana juhudi za kuwapata kutokana na mambo yaliyo nje na uwezo wetu,lakini rai ya wanakijiji hao wameiomba kampuni hiyo kushughulikia jambo hilo haraka iwezekanavyo.

Pia wananchi hao wameiombaplan media  kufikisha ujumbe wao kwa viongozi wa kata hiyo kuwa na dhana ya kushirikiana na wananchi wao kwani mambo yanayowahusu wananchi yanatakiwa yawahusu na viongozi ili kuleta usawa na haki itendwe kwa manufaa ya kata ya Mwandege pamoja nan nchi kwa ujumla katika maendeleo ya kujenga taifa la Tanzania

Chapisha Maoni

0 Maoni