Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

BAISA SASA KIMATAIFA

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania Baisa Mhela aendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa baada ya kupokelewa vyema katika mji wa Mombasa nchini Kenya ambapo amekua na tamasha kubwa la fungua mwaka 2018.

Aidha muimbaji huyo amepata nafasi ya kuendelea kufanya matamasha mbalimbali ambapo anatarajia kufanya tamasha kubwa sana mapema mwezi wapili kwaka 2018 katika mji wa Mombasa nchini Kenya.

Vilevile Baisa amesema kuwa anafurahia mapokezi mazuri kwa wakazi wa Mombasa ambapo hivi sasa anaishi na wenyeji kama mzawa ikiwa ni tofauti na mwanzo ambapo alikua akilala kwenye hoteli jambo ambalo lilikua linamgharimu kiasi kikubwa cha pesa.

Hata hivyo Baisa ameahidi mambo mazuri kutoka Kenya kiwemo kufanya video ya wimbo wake mpya wa JUST, kufanya wimbo mpya kwa kumshirikisha msanii kutoka nchini Kenya pamoja na kuingia mikataba na kampuni kadhaa ambapo ataweka bayana hapo baadae kidogo mambo yakisha kamilika.

Baisa amemaliza kwa kuwaomba wau wadau wa muziki wa injili kuendelea kumuombea pamoja na kufuailia kazi zake ikiwemo nyimbo zake kwa utukufu wa Mungu ili kuikuza huduma yake ya kuihubiri injili kwa njia ya nyimbo kwa mataifa zaidi ya alipo fikia sasa.


TANGAZA NA PLANMEDIA LEO:
+255 713 305 650

planmediatz@gmail.com

Chapisha Maoni

0 Maoni